0



πŸ“ ARUSHA.

Taasisi ya Sayansi ya Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela imempokea mkuu mpya wa Taasisi hiyo baada ya aliyekuwa mkuu wa Taasisi hiyo Mh. Mohamed Gharib Bilal Makamu wa Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumaliza muda wake.

Katika hafala ya makibidhiano iliyofanyika chuoni hapo jijini Arusha makamu mkuu wa Taasisi mstaafu Dkt. Mohamed Bilal amekishukuru Chuo hicho kwa muda wote wa utumishi wake, akiwa ndiye Mkuu wa Taasisi wa kwanza tangu kuanzishwa kwake.

Pamoja na hilo amemuomba Mkuu mpya wa chuo Mh. Omari Issa kuwa kuendeleza yale yote mazuri ili kuweza kukipaiwha chuo hicho.

Aitha Mkuu Mpya wa Chuo Mheshimiwa Omari Issa amemshukuru aliyekuwa mkuu wa Taasisi hiyo Dr. Mohamed Bilal kwa muda wote wa uongozi wake kwa kukiwezesha Chuo kufikia hatua kubwa na kuifanya Taasisi ya Nelson Mandela kuwa moja ya Taasisi kubwa barani Afrika.

Habari zaidi katika picha.
PICHA ☝🏾: Wakuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela pamoja na viongozi waandamizi mara baada ya kuingia katika ukumbi wa mikutano wa chuo hicho.

 
PICHA ☝🏾: Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela Dr. Mohamed Gharib Bilal (aliyesimama kwa nyuma kulia) akimvisha joho ikiwa ni hatua ya kukabidhi ofisi kwa mkuu mpya wa Taasisi hiyo Mh Omari Issa (katikati)

PICHA ☝🏾: Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela Dr. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akiangalia kwa makini jinsi mkuu mpya wa Taasisi hiyo Mh. Omari Issa, akiwekwa vyema vazi hilo na Prof. Ernest Mbega (kushoto)


PICHA ☝🏾: Aliyekuwa Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela Dr. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akifurahia hatua ya kukabidhi madaraka ya ukuu wa Taasisi hiyo, mkuu mpya wa Taasisi hiyo Mh Omari Issa aliyevaa Joho.


PICHA ☝🏾: Mkuu Mpya wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela Mh Omari Issa (kulia)  akimvisha joho na kofia, makamu Mpya Mkuu wa Chuo hicho Prof. Kipanyula.


PICHA ☝🏾: Mkuu Mpya wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela Mh. Omari Issa akimkaribisha Makamu mkuu wa Taasisi hiyo Prof. Kipanyula kwenye nafasi yake mpya kiutendaji.


PICHA☝🏾: Katikati ni Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mh. James Mdoe akimwakilisha waziri wa Elimu, (kulia) Mkuu wa chuo aliyemaliza muda wake Dr. Mohamed Gharib Bilal, (kushoto) Mkuu moya wa Chuo Mh Omari Issa.

PICHA ☝🏾: Aliyekuwa mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela Dr. Mohamed Gharib Bilal, akiongea na kuwaaga Viongozi na wakuu mbalimbali wa idara za Taasisi mara baada ya kukadhibi nafasi ya ukuu wa Taasisi kwa mkuu mpya.

PICHA ☝🏾: Baadhi ya viongozi, wakuu wa vitengo katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela wakisikiliza kwa makini.


PICHA ☝🏾: Mkuu mpya wa Taasisi ya Nelson Mandela Mheshimiwa Omari Issa akiongea katika hafla hiyo na kumshukuru kiongozi mtangulizi mwenzake (hayupo pichani) 

PICHA ☝🏾: Aliyekuwa mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela Dr. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) akipokea zawadi ya Joho na kofia alivyokuwa akitumia alipokuwa mkuu wa Taasisi hiyo kutoka kwa mkuu mpya wa Taasisi hiyo Mh. Omari Issa (kulia).

PICHA ☝🏾: Dr. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) akipokea zawadi ya Picha inayoonyesha waasisi wa chuo hicho Mwl. Julius Nyerere -Tanzania na Nelson Mandela -Afrika ya Kusini pamoja na mazingira ya chuo alichokuwa akikitumikia alipokuwa mkuu wa Taasisi hiyo kutoka kwa mkuu mpya wa Taasisi hiyo Mh. Omari Issa (wa tatu kuja kulia.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top