0

📍ZANZIBAR.

 Spika wa Baraza la Wawakilishi (BLW) Zanzibar Mh. Zubeir Ali Maulid ametembelea maonyesho ya wakulima nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dole Kizimbani mjini Zanzibar.

 Akizungumza mara baada ya kutembelea mabanda kadhaa na kujionea maendeleo mbalimbali ya kilimo na uzalishaji mbalimbali amesema, nimeona uzalishaji wa Samaki wa maji baridi kama Sato kuanza kuzalishwa katika maji chumvi, hii ni hatua kubwa katika visiwa vyetu vya Zanzibar.

 Vilevile amewaomba wananchi kutembelea maonyesho hayo kuweza kujionea miche mbalimbali kama Mwembe ambao unaweza kutoa matunda manne ya aina tofauti katika mche mmoja.











👆PHOTO:

Spika wa Balaza la Wawakilishi Mhe.Zuberi Ali Maulid (kulia) akiangalia vipeperushi na kupata maelezo kutoka kwa Meneja mauzo wa NMB kanda ya Zanzibar Muhsin Nahodha (kushoto) alipotembea banda hilo lilipo katika maonyesho hayo.



   👆PHOTO.

Spika wa Balaza la Wawakilishi Mhe.Zuberi Ali Maulid (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kuhusu aina mbalimbali za udongo na jinsi unavyoweza kupimwa kitaalam na kufanyiwa utafiti, kutoka kwa Islam Mohamed Issa, kutoka Taasisi ya utafiti wa kilimo (ZALE)




 👆PHOTO.

Spika wa Balaza la Wawakilishi Mhe.Zuberi Ali Maulid (mwenye suti nyeusi) akisikiliza maelezo jinsi ya kufanya matibabu kwa paka ambaye amefungwa uzazi na kutoendela kuzaa kutoka kwa mtaalam wa tiba za wanyama kutoka kriniki ya mifugo Zanzibar ndugu Rashid Ibrahim (Kulia), Kushoto kwa kwanza ni Mkurugenzi wa wizara ya kilimo Bi. Asha Zahran.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top