0
ARUSHA.
PHOTO: Askofu wa kanisa la kiinjili la kilutheli
nchini Dkt. Fredrick Oneal Shoo akifungua
mkutano kwa hotuba jijini Arusha.
Mkutano mkuu wa Halmashauli ya makanisa duniani (WCC) unafanyika jijini Arusha ambapo Umishionali na Uinjilisti duniani kila wakati unakusanya kwa pamoja makanisa na madhehebu kutoka pembe za dunia ili kujadili, kutafakari na kupeana uzoefu kutokana na Imani inavyosambaa.

Katika mkutano huo unaofanyika nchini Tanzania kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1958,ikiwa ni kila baada ya muongo na unafanyika ikiwa ni kila dhehebu kushirikiana katika ujuzi na majadiliano ya kidini.

Aitha kufanyika kwa mkutano huu hapa nchini, utazingatia changamoto na mbegu za fursa za Afrika ya leo, kwamba inawezaje kuunda teolojia ya utume na mazoezi ya baadaye na jinsi gani Afrika inaweza kuongeza uelewa wa ujumbe kwa namna ya kipekee na ya kibunifu.



Hizi hapa chini ni baadhi ya picha za matukio yaliyojili kwa siku ya leo kutoka Ngurdoto Mountain Lorge jijini Arusha.

PHOTO: Maandamano kuelekea kufungua mkutano yakiongozwa na Mchungaji Dkt. Fredrick Shoo kuelekea kwenye ukumbi wa mkutano uliopo kwenye Ngurdoto Mountan Lodge.
PHOTO: Baadhi ya wahudhuliaji wa mkutano huo wakisikiliza na kuangalia nyimbo zilizokuwa zikiimbwa katika mkutani huo.

PHOTO: Kikundi cha kusifu na kuabudu kikiimba wakati wa kuanza kwa ibada ya pamoja wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.


PHOTO: Askofu mkuu, Dkt. Fredrick Oneal Shoo wa kanisa la kiinjili la kilutheli nchini akiongea wakati wa kufungua rasmi mkutano mkuu wa umoja wa makanisa duniani mapema leo jijini Arusha.

PHOTO: Baadhi ya wahudhuliaji wa mkutano huo wakimsikiliza kwa makini Dkt. Fredrick Shoo (hayupo pichani) alipokuwa akifungua mkutano huo mapema leo

PHOTO: Katibu mkuu wa umoja wa  makanisa duniani Mchungaji, Dkt Olav Fykse Tveit akiongea na wanahabari wakati akijibu swali kuhusu umoja wa makanisa kuwa na Amani na ushirikiano katika kipindi hiki ilihali katika baadhi ya nchi hakuna Amani na baadhi ya serikali kufungia makanisa huku wachungaji wa makanisa wakiwa hawajui la kufanya.



Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top