PWANI.
ELIMU HAINA MWISHO.
Mahafari ya kumi na mbili (12) ya Shule ya
sekondari ya Baobab iliyopo mkoani pwani wilaya ya Bagamoyo yamefanyika shuleni
hapo ambapo mgeni rasmi akiwa Naibu Waziri ofisi ya Nchini, Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleiman Jaffo.
![]() |
PHOTO: Waziri wa Naibu
Waziri ofisi ya Nchini,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(Tamisemi)
Suleiman Jaffo akiongea na kadamnasi
wakiwemo
wahitimu wa kidato cha sita.
|
Katika mahafari hayo ambayo wahitimu wapatao 295
wanatarajia kuhitimu elimu yao ya kidato cha sita katika shule hiyo.
Shule ya sekondari Baobab inayomilikiwa na
Asasi isiyo ya kiserikali ya Shajar School Association ilianzishwa mnamo mwaka
2005 ikiwa na wanafunzi 70 wa jinsia ya kike pekee ambapo baadae uongozi
ulifanya mabadiriko na kuamua kuifanya kuwa mchanganyiko.
Katika sherehe za mahafari hayo Uongozi wa
shule hiyo umeiomba serikali kurekebisha sheria ya aridhi namba 178 ili iruhusu
kubadirisha matumizi ya aridhi lakini pia Serikali iiwezeshe mamlaka ya Elimu
Tanzania (TEA) kutunisha mfuko wa kutoa huduma za mikopo na vifaa kwa shule za
serikali na binafsi ili kuwepo maendeleo makubwa ya Elimu nchini.
Hata hivyo naibu Waziri Suleiman Jaffo
pamoja na kuhusifu uongozi wa shule hiyo kwa mafanikio wanayopata kutokana na
ubora na elimu wanayotoa shule iyo, amewataka kuweka nafasi stahiki kwa mzazi
yeyote kuweza kumleta mwanaye pasi kuwepo vipingamizi.
Katika kujibu risala iliyotolewa kwake
amesema, serikali ipo bega kwa bega na sekta binafsi katika maendeleo ya Elimu
nchini na ndiyo maana inaendelea kutoa fulsa kwa Mtanzania mwenye uwezo wa
kuwekeza kwenye sekta hiyo.
"serikali tutaangalia ni jinsi gani tunaweza kuzisaidia
mamlaka zinazohusika na elimu kama TEA kuweza kufanikisha malengo ya kunyanyua
elimu yetu nchini" alisema
Suleiman Jaffo.
Kwa upande mwingine mdau wa elimu ambaye
pia ni Mbunge wa viti maalum Esther Alexanda kutoka Manyara ambaye pia ni
mwenyekiti wa shule binafsi nchini ameiomba serikali wawekezaji kupitia elimu
hawaleti mvutano ktk nyanja hiyo bali wanaomba ifanye Public Private
Partnership (PPP) "kwenye sekta ya Elimu kama ilivyo kwenye sekta ya Afya
ili kuwepo na maendeleo kwa upande huo"
![]() |
PHOTO: Naibu
waziri (Tamisemi) Suleiman Jaffo (katikati), Mkurugenzi mkuu wa shule za Baobab
(kulia) na viongozi wengine wakiimba wimbo wa taifa wakati wa sherehe hizo.
|
![]() |
PHOTO:
Mdau wa elimu ambaye pia ni Mbunge wa viti maalum Esther Alexanda kutoka
Manyara
|
![]() |
PHOTO:
Mkurugenzi mkuu wa shule za Baobab akiongea wakati wa sherehe hizo na kabla
hajamkaribisha naibu waziri wa Tamisemi Suleimani Jaffo (pichani kulia)
|
![]() |
PHOTO: Baadhi
ya wahitimu wa kidato cha sita wakimsikillza Mkurugenzi mkuu wa shule hizo (pichani juu) akiongea kwenye sherehe hizo.
|
![]() |
PHOTO: Wahitimu wa kidato cha sita wakisoma risala yao kwa naibu waziri wa Tamisemi (hayupo pichani)
|
![]() |
PHOTO:
Mkurugenzi mkuu wa shule za Baobab akimkakabidhi naibu waziri wa Tamisemi Suleimani Jaffo (kulia) risala ya shule.
|
![]() |
PHOTO: Naibu
waziri (Tamisemi) Suleiman Jaffo (katikati) akiongea mara baada ya risala iliyosomwA kwake.
|
![]() |
PHOTO: Baadhi
ya wahitimu wa kidato cha sita wakimsikillza Naibu waziri Suleimani Jaffo (hayupo
pichani) wakati akitoa hotuba kwa wanafunzi, ndugu, jamaa, walimu waliofika
katika sherehe hizo.
|
![]() |
PHOTO: Naibu waziri (Tamisemi) Suleiman Jaffo (aliyeshika kipaza sauti) akiwatunuku vyeti wanafunzi wanaohitimu elimu ya kidato cha sita, pichani chini.
|
PHOTO: Baadhi
ya wahitimu wakinyanyua juu vyeti vyao kuonyesha furaha ya kuhitimu elimu ya
sekondari wkt wa kukabidhiwa na naibu waziri shuleni hapo Bagamoyo Mkoani
Pwani.
|











Post a Comment