GEITA.
Mamia ya wananchi, viongozi wa CCM na matajiri wakubwa wa mji wa Geita
wamemiminika katika viunga vya mahakama ya hakimu mkazi Geita wakisubiri
kupandishwa mahakamani kwa Mbunge wa Geita Vijijini, Joesph Msukuma na madiwani kumi wanaoshikiliwa
na jeshi la polisi kwa kusababisha vurugu zilizotokea Septemba 14 mwaka huu.
![]() |
| PHOTO: Mbunge wa Geita Vijijini Msukuma. |
Walianza kufika mahakamani majira ya
saa nane mchana wa leo Jumatatu baada ya taarifa kuanza kuenea kuwa
watapandishwa mahakamani lakini hadi kufika majira ya saa 9:20 alasiri Katibu
wa CCM Mkoa wa Geita, Adam Ngalawa akatangaza kuwa viongozi hao hawatafikishwa
tena mahakamani kutokana na muda wa Mahakama kumalizika.
“Tulikua tunawasubiri wenzetu tuwawekee dhamana lakini
nimepigiwa simu sasa hivi kuwa hawataletwa tena mahakamani kwa kuwa muda wa
Mahakama umekwisha na taarifa nilizopokea tumeambiwa wataletwa kesho,” amesema
Ngalawa.
Wakizungumza baada ya kauli ya
katibu kuwa viongozi hawataletwa mahakamani baadhi ya wafuasi Ikorongo Otto na
Masanja Malembeka wamesema kwa sasa hofu imetanda kwa wananchi kwa kuwa huo
haukuwa utamaduni uliozoeleka wa kuona viongozi wanakamatwa wakiwa wanadai mali
zao.
Awali akizungumza na waandishi wa
habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Mponjoli Mwabulambo
amesema wote wanaoshikiliwa bado wako ndani na watafikishwa mahakamanil leo
hata kama muda wa mahakama utakuwa umekwisha watamuomba hakimu.
Amesema dhamana za watuhumiwa ziko
wazi kwa kua ni haki ya mtuhumiwa lakini akasema dhamana hiyo inategemea na
mazingira ya tukio.
Kamanda amesema bado zoezi la
kuwakamata madiwani waliokimbia linaendelea na kuwakata wasiwe wakimbizi badala
yake warudi kwenye familia zao kwa kuwa kosa la jinai halina mwisho na lazima
watakamatwa kwa uvunjifu wa sheria.
CHANZO:
![]() |
| PHOTO: Walipokuwa wamefunga barabara. |
Mbunge Msukuma na
madiwani wa wilaya ya Geita walifunga barabara zinazoingia kwenye mgodi wa GGM
wakishinikiza kulipwa dola 12 milion zinazotokana na kodi ya huduma.
Kamanda wa polisi
mkoani hapa Mponjoli Mwabulambo amethibitishwa kukamatwa kwa Msukuma na kusema
askari walimkamata katika eneo la CCM mjini Geita.
Source: Mwananchi.


Post a Comment