DODOMA.
Wakati Bunge likiendelea mjini
Dodoma, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai,
amesema ana uwezo wa kumzuia Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe kuzungumza
mpaka mwisho wa bunge, kwani hawezi kupambana naye.
![]() |
Profile PHOTO: Spika John Ndugai. |
Spika Ndugai ametoa kauli hiyo
Bungeni leo huku akisema Zitto Kabwe hawezi na hapaswi kujibizana naye na amemtaka
Zitto kutomfananisha na aliyekuwa Spika wa Bunge marehemu Samuel Sitta, kwani
hawezi kufanana naye na kila mtu ana zama zake, kama ambavyo Spika wa bunge
aliyepita mama Anna Makinda alivyokuwa na muda wake kuliongoza bunge hilo.
"Hawa ni watu ninaowaheshimu na wamenilea sana na ni sehemu ya
nilipofika hapa leo, utanilinganishaje mimi na milima mikubwa kama Kilimanjaro?
Hata siku moja sikio haliwezi kuzidi sikio," amesema
Ndugai.
Amesema katika Bunge la 9 Zitto
aliwahi kupeleka hoja ya Mgodi wa Buzwagi ambayo ilikataliwa na Bunge lakini
ikazuka hoja ya kimaadili ambapo alihukumiwa papo kwa hapo.
"Alihukumiwa papo kwa hapo akapigwa miezi mitatu, yaani mnataka
niende mkuku mkuku kama lile la Bunge la tisa nifanane na mzee Sitta?, hilo pia
naliweza kwa nini mnaalika matatizo nashangaa unapambana na Spika, mimi ninauwezo
wa kupiga marufuku kuzungumza hadi miaka yote mitano iishe hauna pa kwenda,
hakuna cha swali, nyongeza wala kuzungumza utanifanya nini? Alioongeza
Ndugai.
![]() |
Profile: Zitto Kabwe akiwa Bungeni |
Kufuatia kauli hiyo spika
Ndugai amemtaka kupambana na mtu mwingine lakini sio yeye."Kwa haya ya Spika sina sababu nayo lakini ya kulidharau bunge
hayo sitaweza kuyavumilia nitalinda mihimili huu kwa nguvu zangu zote," amesema.
Amesema hawawezi kuacha wabunge
kulidhalilisha Bunge na kuhoji kwamba watachukuliaje Watanzania wengine
watakapolidhalilisha Bunge, amesema hilo kosa la pili kwa Zitto na kuagiza
liende katika kamati ya maadili.
Siku ya jana Spika Ndugai
alimtaka Zitto Kabwe kufika kwenye kamati ya maadili kutoa maelezo juu ya taarifa alizoziweka kwenye
mtandao, na Zitto Kabwe kumjibu kuwa mambo anayoyafanya Spika yanaporomosha
bunge.
"Tutaenda sambamba mguu kwa mguu hadi kieleweke," aliongeza Ndugai
Post a Comment