0
DAR ES SALAAM.
Shirika lisilo la kiserikali la Twaweza limetoa tafiti inayoangazia utolewaji wa taarifa kwa umma ikionyesha kuwepo kwa ukinzani kwa maofisa wa serikali kutokuwa na ushirikiano kwa wananchi na wadau wa habari ikizingatiwa kuwa utolewaji wa habari ni haki kwa kila mwananchi kupata na kupewa taarifa.

PHOTO: Kajibu Mukajanga akiongea na wanahabari
(hawapo pichani) kuhusu tafiti ya haki ya
kupata habari kwa wananchi.
Akikizungumza wakati wa mjadara huo Kajubi Mukajanga ambaye ni meneja wa Twaweza amesema sheria ya kutoa taarifa imepiganiwa kwa muda mrefu mpaka kupatikana ila inashangaza kuona baadhi ya vyombo vya serikali havitoi taarifa “tunaiomba serikali ihakikishe sheria ya kupata taarifa inafanya kazi, maana sheria hii ndiyo itaweza kumpa nafasi mwanchi kwenda sehemu yoyote au katika idara yoyote na kutaka apewe taarifa maendeleo ya watu” alisema Mukajanga

Sheria hiyo iliyopitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais mwaka mmoja uliopita inaonekana kutoanza kutumika kwa sababu zisizofahamika, hata hivyo hakuna ofisa yeyote wa serikali anayeweza kuizuia kufanya kazi kwa kutokutimiza wajibu wake.
Aliongeza kuwa “vinginevyo itakuwa ni danganya toto hauwezi kuwa na sheria iliyopitishwa na bunge na kusainiwa na Rais eti haifanyi kazi kwa sababu watendaji flani hawajatimiza wajibu wao”.

Wakati Tanzania ni  miongoni mwa nchi chache zenye sheria ya kupata taarifa duniani bado sheria hiyo haijawekwa katika gazeti la serikali ili iweze kutumika rasmi hivyo kuwakosesha 80% ya watanzania wanaojua wana haki ya kupata taarifa.

PHOTO: Meneja utetezi Ananstazia Rugaba akiongea
kuhusu wakati kutoa tathimini kwa vyombo vy habari.
Meneja wa mradi huo Anastazia Rugaba ameiomba serikali kuwashirikisha wadau ili kutengeneza kananu zitakazosaidia sheria hiyo iweze kuanza kufanya kazi ambapo itatoa nafasi kwa wananchi kwenda katika ofisi au idara yoyote kupata taarifa.

“kila ofisi ya serikali ina kitengo cha kutoa taarifa lakini bado maofisa wa hivi vitengo wamekuwa ni wagumu wa kutoa taarifa na  wananchi wanaamini kupewa taarifa zozote isipokuwa zile za usalama wa taifa, na hata wale wenye uwezo wa kutoa taarifa hawana nyezo, rasilimali za kuwafanya watoe taarifa” amesema Anastazia Rugaba.

Hata hivyo utafiti huo unaonyesha kuwa katika maombi matatu ya kuomba kupata taarifa ni moja ndilo lilijibiwa, huku wakipewa muda mrefu wa kupata majibu na baadhi ya idara za serikali kama taasisi za elimu na vitengo vyake ikiwemo wizara ya Afya haikuwa raisi kupata taarifa.


Pamoja na hayo ofisi za Aridhi, Maji na Mipango kwa wastani walijitahidi kutoa taarifa.

Post a Comment

 
Top