DAR ES SALAAM.
![]() |
PHOTO: Mwenyekiti wa cha
walemavu wa mtindio
wa ubongo Hilal Said
akiongea na wanahabari
(hawapo pichani)
kuhusu athali
wanazokumbana nazo wanachama wao.
|
Chama cha walemavu wa
mtindio wa ubongo nchini kimetoa wito kwa serikali kutoa fulsa sawa kwa watu wa
kada hiyo ili kuweza kuweka usawa na kuepusha lawama za mara kwa mara
zinazotolewa na kada hiyo, ambayo imeonekana kutoweza kufanya kazi yoyote ya
uzalishaji.
Akiongea na wanahabari
leo jijini Dar Es Salaam mwenyekiti wa chama hicho Hilal Said amesema kuwa,
pamoja na kuwepo kwa chanamoto kwa walemuvu hao hapa nchini kutoweza kufanya
kazi zote bado nafasi ya kuwaamini ipo na kwa kadiri wanavyoweza kujituma katika
maisha yao ya kila siku.
Ameongeza kuwa wao kama
walemav wanayo haki kama watu wa kada nyingine na uwezo wao kufanya kazi za kila
aina upo ili mradi miundo mbinu iwepo ya kutosha, “mara nyingi watoto wenye mtindio wa ubongo
wanantengwa na jamii hata ikifikia mzazi mmoja akifariki akibaki mama kupata mwenzi
inakuwa vigumu” amesema
Mawanahamisi Hussein.
Ugonjwa wa mtindio wa
ubongo ni athali inayotokea kwenye ubongo ambao wa kuendelea, mara kadhaa
uonekana katika misuli ambayo usababisha ulemavu na mara nyingi athari hii
ujitokeza zaidi kadiri mtoto anavyokuwa.
![]() |
PHOTO: Kutoka kushoto ni Jane Kumu Mtunza hazima wa chama, katikati Hilal Said mwenyekiti na kulia ni Mwanahamisi Hussein katibu wa chama |
Naye katibu wa chama
hicho Mwanahamisi Hussein amesema, pamoja na kuwepo kwa unyanyapaa kwa watu hao
bado kumekuwepo kwa baadhi ya jamii hasa wanaume kutooa mwanamke ambaye katika
jamii yake au mtoto wake anaugonjwa huo.
“unyanyasaji wa jamii hasa kwa sisi wanawake ambao tumeondokewa
na mume na kubaki na mtoto mwenye ugonjwa huu bado ni mkubwa kutokana na
wanaume wengi kuona mzigo endapo atahamu kuoa mwanamke mwenye mtoto aliye na ugonjwa
wa mtindio wa ubongo” amesema Mwanahamisi.
Post a Comment