DODOMA.
Taasisi
isiyokuwa ya kiserikali inayofanya utafiti kwatika nyanja mbalimbali za kijamii
na kuishirikisha jamii katika utafiti hapa nchini TWAWEZA imetoa utafiti unaoonyesha muelekeo
miongoni mwa watoto wenye umri wa miaka 9 mpaka 13 wengi wao hawawezi kufanya
majaribio ya kiwango cha darasa la pili (Std 2).
Katika utafiti
uliofanyika katika mikoa kadhaa inaonyesha asilimia 42 ya watoto kutoka kaya
kasikini walifaulu majaribio ukilinganisha na asilimia 58 kutoka kaya tajili, hali
hizi zinaonyesha kuwa mahali anaposhi mwanafunzi panachangia kwa kiasi kikubwa
katika matokeo ya kujifunza kuliko hali ya kiuchumi na vitu vingine ambavyo
uhusika katika kuleta Elimu.
![]() |
PROFILE PHOTO: Mkurugenzi TWAWEZA Aidan Eyekuze. |
Mkurugenzi mkuu wa
TWAWEZA Aidan Eyekuze anasema “inatia moyo kuona watoto wetu wanapata matokeo mazuri
zaidi kuliko miaka ya nyuma kwenye somo la Kiswahili, lakini safari bado ni
ndefu. Kitu cha kutia shaka ni ongezeko la kukosekana kwa usawa kwenye matokeo
ya kujifunza kutokana na maeneo wanayoishi watoto, kwani takwimu zinaonyesha
mahali anapoishi mtoto panachangia kwa kiasi kikubwa uwezo wake wa kujifunza
kuliko sababu nyingine ama kutokupata elimu ya mama yake au kutokuoata elimu ya
awali.”
Aitha ripoti hiyo
imetoa matokeo ya jumla katika kuoanisha uwezo, na jitihada za wanafunzi katika
kusoma na kufanya hesabu, lakini pia imeonyesha wanafunzi wengi walio katika
madarasa ya chini wapo nyuma ya matarajio ya mtaala pamoja na hali hiyo kutia
matumaini.
Kwa upande mwingine
ripoti imebainisha kushuka kwa kiwango cha uandikishaji wa watoto wa vijijini hasa
katika miongoni mwa rika zote wakati kwenye maeneo ya mijini umeendelea kuimarika.
Zaida Mgalla, Meneja
uwezo Tanzania anasema “Tunaipongeza serikali kwa jitihada zake za kuhakikisha
watoto wanapiga hatua katika somo la Kiswahili pamoja na kuhakikisha watoto
wengi wanapata vitabu, lakini hatupaswi kuridhika, kwani changamoto
inayotukabili sote ni kuhakikisha tunapiga
hatua katika kuelekea ubora uliokusudiwa katika sekta ya Elimu, na kwa
kujikita zaidi katika kuboresha matokeo ya kujifunza katika shule zetu”
Post a Comment