0
DAR ES SALAAM.
Msanii Roma Mkatoliki asema anahofia maisha yake siku moja tu baada ya kupatikana katika kituo cha polisi cha Oysterbay.


Akizungumza na vyombo vya habari akiwa na waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, Roma mkatoliki ameelezea jinsi walivyotekwa siku ya Jumatano na kufungwa pingu, kitambaa usoni na baadaye kusafirishwa hadi eneo wasilolijua.

PHOTO: Msanii Roma Mkatoliki kulia akiwa na Waziri
Dr. Harison Mwakyembe kulia.

Akizungumza kwa hisia na uchungu Roma alisema kuwa walipofikishwa walipopelekwa na kupata mateso mengi kwa kupigwa hadi siku ya Ijumaa usiku.
“Tukatolewa tulimokuwepo siku ya ijumaa jioni na kufungwa uso, na mikono na miguu. Tukapelekwa sehemu tukatupwa kwenye dimbwi la maji karibu na baharini Roma anasema kuwa alipata fahamu na kuweza kuwafungua wenzake na kutembea mwendo mrefu ambapo walifika katika maeneo ya Ununio” alisema Roma Mkatoliki
Hata hivyo msanii huyo alishindwa kuelezea baadhi ya maswali aliyoulizwa kuhusu kile walichokuwa wanaulizwa na watekaji huku akisema kwamba tayari wamewasilisha malalamiko yao polisi kwa uchunguzi, huku maofisa wa serikali walioandaa mazungumzo hayo na wanahabari wakimzuia msanii huyo kusema lolote .
Katika mkutano huo Roma na wenzake walionyesha baadhi ya majeraha waliyopata chini ya watu waliowateka na kusisitiza kwamba kile walichokipitia sio suala la mzaha, wameitaka serikali kuwahakikishia usalama wao wakidai kwamba licha ya kuwepo katika eneo lililozungukwa na watu maarufu ikiwemo serikalini watekaji wao walifanikiwa kutekeleza tendo hilo bila wasiwasi.

Post a Comment

 
Top