Na
Mary Mwakibete –Mbeya.
Mkuu
wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla amepokea msaada wa mifuko ipatayo 400 ya saruji
ikiwa ni hatua moja kutokana na ombi lake kwa Benki ya Akiba Commercial Ltd nchini
tawi la Mbeya kusaidia ujenzi wa Hospitali ya rufaa kwa upande wa njia za
wagonjwa zenye umbali wa mita 175.
![]() |
PHOTO: Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla
Akiongea wakati
katika hafla fupi ya
kupokea msaada wa mifuko ya saruji jijini Mbeya,
kulia kwake ni Afisa
masoko na uendeshaji wa Akiba Dora Saria.
|
![]() |
PHOTO: Afisa masoko na Uendeshaji Dora Saria
(wa kwanza kushoto) akongwa jambo wakati wa kukabidhi msaada wa saruji kwa mkuu
wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla mwenye miwani.
|
![]() |
PHOTO: Mmoja wa wafanyakazi wa benki Akiba
akipokea mfuko wa saruji kutoka kwenye roli ili kuukabidhi kwa RC Makalla.
|
>>>>>>>>
Katika hafla fupi ya
makabidhiano hayo, RC Makalla amewapongeza na kuushukuru uongozi wa Benki hiyo
kwa jinsi walivyojitoa na kushugulikia maombi kwa haraka na kusaidia kuendeleza
ujenzi uliokuwa umesimama kutokana kukosekana kwa fedha shilingi 55 milioni, hivyo
msaada huo utakuwa na tija kwa mkoa wa Mbeya na ukanda mzima wa nyanda za juu
kusini na nchi kwa ujumla.
Aitha Mkuu huyo wa Mkoa
kupitia kwa marafiki wa hospitali ya mkoa wale wanaoishi nje ya mkoa huo
wamekamilisha ujenzi wa mita 155 kupitia harambee iliyofanikisha ujenzi huo,
ambapo katika ujenzi huo fedha zilizotumika ni shilingi 160 milioni za
Tanzania.
“Kukamilika kwa ujenzi huu kutaondoa tatizo la wagonjwa
kupelekwa au kwenda wodini kupita kwenye mazingira yasiendana na hali ya
mgonjwa, pia wakati wa mvua na jua tatizo linakuwa kubwa” alisema RC Makalla.
Kwa upande mwingine
afisa masoko na uendeshaji wa Benki ya Akiba Dora Saria amesema kutokana na
wananchi kupata shida hasa wagonjwa kwenda wodini au kupeleka maiti kwenye chumba
cha kuhifadhia marehemu kutokuwepo na njia rafiki, wao kama benki inayotoa
huduma kwa wananchi waliguswa na kutokana na ombi la Mkuu wa Mkoa ambapo
wamechangia shs 5milioni ambayo ni sawa na mifuko ya saruji 400.
Pia benki imevutiwa na
jitihada za mkuu wa mkoa katika kuliweka jiji la Mbeya katika mazingira safi
hivyo watatoa vifaa vya usafi na kushiriki kufanya usafi mwishoni mwa mwezi
huu.



Post a Comment