![]() |
| PROFILE CARTOON: Sudani kusini alipokuwa anaomba kujinga na EAC. |
Bunge la afrika mashariki limeweka
wazi, suala la kuzorota kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika uwasilishaji
na utoaji wa michango ambapo kutokana na hilo wameonya kuwa ikiwa hatua stahiki
hazitachukuliwa haraka jumuiya hiyo itaelekea pabaya.
Baadhi ya mambo yanayochangia ni kutotekelezwa
kwa miradi mbalimbali ya maendeleo, kutolipwa mishahara wafanyakazi wa jumuhiya
hiyo kwa muda sasa, hizo ni baadhi ya changamoto zilizopo na zimeanza
kujitokeza kutokana na nchi hizo kutochangia kwa wakati.
![]() |
| PHOTO: Bendera za nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki |
Wabunge hao wamesema ingawa kumebaki
miezi kadhaa ili mwaka wa fedha uishe, mchango uliotolewa haufikii hata nusu ya
bajeti inayotakikana, hilo ndio limewafanya wabunge hao kuomba serikali za nchi
wanachama kutoa maelezo na kutekeleza swala la utoaji wa michango kwani
changamoto zinazidi kuongezeka.
Aidha licha ya mengi yaliyozungumzwa katika mkutano huo wabunge hao wamewaagiza mawaziri wa jumuiya ya Afrika Mashariki kujadili haraka pamoja na viongozi wakuu wa nchi hizo ili kutatua jambo hilo.
Kwa upande wao mawaziri ambao pia
wameudhuria vikao vya bunge wametangaza kwamba suala hilo linaenda kupewa uzito
na muda si mrefu litajadiliwa na viongozi wa nchi. Wabunge hao wamesema
serikali zinapaswa kujihadhari ili Jumuiya isije kuvunjika tena.
Source: rfi


Post a Comment