0
PHOTO: Mwanasheria Laurence Masha ambaye amejitoa
kugombea nafasi ya Urais wa TLS na kumuunga
mkono mgombea mwenzake Tundu Lissu.
ARUSHA.
Hatimaye wakati wa kujinadi na maswali ulifika kwa wagombea kuweka bayana maslahi yao kwa chama hicho cha watetezi wa raia katika vyombo vya kudai haki, ambapo wagombea walikuwa sita mmoja kati yao Laurence Masha yeye aliamua kujitoa na kumuunga mkono Lissu kwa maslahi chama na wanachama wengine akidai kwa sasa chama kinataka mtu mwenye nguvu na uwezo wa kukisaidia katika kusimamia haki.

Aitha wakati wote wa kujinadi kwa mgombea mmoja mmoja, aliyeonekana kukonga mioyo ya wanasheria hao kila alipokuwa akiongea alipigiwa makofi lakini hali ilikuwa ya hamasa hasa pale aliposimama Tundu Lissu.

TODAYS NEWS tunakuwekea video ambayo Lissu aliweza kujieleza, kujinadi na kujibu maswali kadhaa hapo jana jijini Arusha ilikuwa muda mfupi tu alipofika kutokea Dar Es Salaam, alipokuwa ameshikiliwa na jeshi la polisi kisha kupewa dhamana.



Post a Comment

 
Top