![]() |
| Profile PHOTO: Mshare ukielekeza kwenye mabadiriko. |
Uchafuzi
wa hali ya hewa umeendelea kutajwa kuwa changamoto ambazo zimeendelea
kuzikabili nchi nyingi barani la Afrika ambapo kwa mujibu wa shirika moja la
umoja wa Mataifa linaloshugulikia mazingira, limezitaka nchi za Afrika kuwekeza
katika miundombinu ili kuweza kuwaruhusu wananchi kutembea kwa miguu au kutumia
aina ya usafiri wa baiskeli.
Matumizi ya kutumia miguu na baiskeli itakuwa mojawapo ya njia itakayoweza kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa
unaotokana na matumizi ya usafiri wa magari, vyombo vya moto vinavyotumia
mafuta ya petroli au dizeli vinatoa gesi joto ambayo inachangia kwa kiasi
kikubwa katika kuongezeka kwa joto dunianil.
![]() |
| PHOTO: Mabadiriko ya mazingira na Athali zinazoikabili dunia. |
Katika
bara la Afrika ujenzi wa miundo mbinu kama ya barabara mfano katika jiji la Dar
Es Salaam na Arusha inaonyesha kuwepo na njia zitakazoweza kutumika kwa watu
watakaotumia miguu au baskeli ambazo hazitumii mafuta yoyote yale hivyo haina
mchango wowote katika uchafunzi wa mazingira, lakini matumizi ya baiskeli hama
na kutembea kwa miguu hubolesha Afya za wananchi, sababu iankuwa ni sehemu ya
mazoezi
Kuna
nchi ambazo ni hatari zaidi unapotembea kwa miguu au kwa kutumia usafiri wa
baiskeli, Malawi ni nchi ya kwanza kwa mtu kutumia usafiri huo huku ikifuatiwa
na Kenya ya tatu ni Afrika Kusini ambapo katika utafiti uliofanywa hivi
karibuni umeonyesha kutokuwepo kwa njia za watembea kwa miguu au waendesha
baiskeli hivyo mazingira hayo yanaweka ugumu kwa raia wa nchi hizo kutokuwa
salama wanapotembea au kutumia baiskeli.
Kwa msaada wa rfi


Post a Comment