0
Warsha ya mafunzo namna ya kushugulikia kesi na matatizo ya ukatili, unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto, imefunguliwa jijini Arusha ikiwa ni mafunzo ya kipekee kwa wakati huu ambapo ambapo matendo ya ukatili wa kijinsia yamekithiri kwa kiasi kikubwa katika jamii hapa nchini.


ARUSHA.

PHOTO: Mkuu wa wilaya ya Arusha Fabian Daqarro.
Akifungua mafunzo hayo, kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, Mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Fabian Daqarro amesema wakati kuna sheria mbalimbali za kitaifa na kimataifa zikiwepo nyingine ambazo zitasaidia kuongeza uelewa na ufahamu wa jinsi ya kushugulikia kesi za ukatili wa kijinsia mafunzo hayao yawe ni msaada wawapo mahakamani ili kuongeza ufahamu na kuweza kusaidia kuboresha ufanisi wa kazi mahakamani na kwenye jamii.


“Mafunzo haya yanalenga kuangalia namna gani mahakimu na majaji wanawake wanaweza kuongezewa ujunzi, mafunzo na namna ya kwenda kushugulikia haya matatizo sugu katika jamii yetu, sababu hata hapa wilayani kwetu Arusha haya matatizo yapo ya watoto kulawitiwa, kubakwa, kudhalilishwa, kupigwa, kuonewa, mirathi  na kunyang’anywa mali haya ni matatizo ambayo kupitia mafunzo haya tutapata msaada kuweza kutatua hali hii” amesema Daqarro.


PHOTO: Iman Aboud, Mwenyekiti wa chama
cha majaji na wahakimu wanawake nchini.
Mafunzo hayo yameshirikisha viongozi mbalimbali kutoka sekta za kijamii, wasimamizi wa sheria, polisi, mawakili wa serikali na wakujitegemea, vyombo vya usalama, watoa haki majaji na mahakimu pia wakiwepo viongozi wa dini, lengo likiwa ni kuwapa uwezo katika kushugulikia masuala ya kijinsia na ukatili.

Jaji na Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania Iman Aboud anasema huu ni muendelezo wa jitihada zilizoanza toka mwaka 2000 ambapo chama kilianza huku jitihada ikiwa ni kumfanya mwananchi kutambua haki zake hasa pale anapofanyiwa ukatili na namna gani atamtetea mtoto wake hama mirathi yake.

Jaji Aboud anasema “washiriki katika warsha hii pia tumewajimuisha viongozi wa dini mbalimbali tukiamini kabisa nao wanapokuwa katika nafasi zao kama watu wanaojenga jamii, wakizungumza katika sehemu zao misikitini, makanisani watasaidia sana, na sisi kama wanawake tunalichukua jambo ili kwa uzito mkubwa ukizingatia sisi ni wana taaluma siyo wana harakati ndiyo maana tunajikita katika kutoa Elimu, na tunatoa elimu tukizingatia ukomo ambao sisi kama majaji tunakuwa nao”.

Warsha hiyo ya siku tatu inategemewa kuwa msaada kwa washiriki wa mafunzo kuwapa njia itakayoweza kuifanya jamii kuwa na uelewa wa namna ya kujilinda na kujikinga dhidi ya unyanyasaji unaofanyika katika jamii, hata hivyo mafanikio yanayotokana na mafunzo haya mpaka sasa yanaonekana ni makubwa kutokana na maamuzi yanayofanywa sasa na vyombo vinavyotoa haki kuonekana kutoka katika ngazi ya chini.


PHOTO: Picha ya pamoja kwa washiriki wa mafunzo ya kushugulikia kesi na matatizo ya ukatili, unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto, waliokaa wakiongozwa na mkuu wa wilaya ya Arusha Fabian Daqarro (mwenye tai) kulia kwake ni Jaji Iman Aboud na Jaji Mstaafu Eusebia Munuo na Kushoto kwa mkuu wa wilaya ni Jaji Sekera Moshi.


Post a Comment

 
Top