0
PROFILE PHOTO: DR CONGO
Maofisa wa Jeshi la polisi wapatao 40 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameuawa kwa kukatwa mapanga na wanamgambo wa kundi la Kamwina Nsapu katika jimbo la kati la Kasai ijumaa ya juzi.

Kwa mujibu wa rais wa bunge la Kasai Francois Kalamba, wanamgambo hao waliushambulia msafara wa magari ya polisi uliokuwa njiani kutoka mji wa Tshikapa kuelekea mji mkuu wa jimbo la Kasai wa Kananga waliposhambuliwa  wanamgambo hao.

Kalamba amesema walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa wanamgambo waliwaachia huru maofisa sita kwa vile walikuwa wanazungumza lugha ya Tshiluba inayotumika eneo hilo, pia wanamgambo hao ambao kawaida huwa na mapanga, waliiba bunduki na silaha za polisi kisha na kukimbia pamoja na magari yao.


Uasi katika eneo la kati ya nchi ya DRC ulianza mwezi Agosti mwaka uliopita 2016 na umeenea katika majimbo kadhaa ya eneo hilo. Hata hivyo siku ya (jana) Jumamosi wizara ya mambo ya ndani ya serikali ya nchi hiyo imetangaza kwamba kuna wanamgambo 400 wamejisalimisha kwa wiki hii katika jimbo hilo la Kasai.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top