0
Na Humphrey Polepole.   -I
Hivi karibuni kumekuwapo maneno ya upotoshwaji juu ya Mabadiliko ya Katiba ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yaliyofanyika tarehe 12 Machi 2017. Napenda kufafanua kwa uchache maeneo ambayo yamefanyiwa Mabadiliko ili kuanzia sasa ieleweke bayana kwamba msingi wa Mabadiliko haya ni Mageuzi Makubwa ambayo yanafanywa na Chama chetu ili kuongeza tija, ufanisi, uwajibikaji, kupunguza gharama za uendeshaji, kupiga vita rushwa na ubadhirifu wa mali za umma.

Mageuzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yanalenga kutizama Uongozi (Leadership), Muundo/Mfumo (Structure/System) na Utawala (administration). Chama chetu kimetimiza miaka 40 mwaka huu (2017) tangu kuanzishwa kwake na kipindi hiki tumeazimia kwa kauli moja kukiimarisha, kukijenga na kukifanya madhubuti. Kazi hii ya Mageuzi ya CCM ilianzishwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM iliyokaa katika Mkutano wake wa mwenzi Desemba 2016 na baadaye kupitishwa kwa sauti moja na Mkutano Mkuu Maalum wa Machi 2017.

Ikumbukwe kwamba mabadiliko haya ya Katiba yangaliweza kupendekezwa na kuanza kutumika pasina ya kuitisha Mkutano Mkuu, lakini hekima ya Uongozi wa Chama chini ya Mwenyekiti Ndugu Magufuli na Katibu Mkuu Ndugu Kinana ikatuongoza kwamba Mabadiliko haya ambayo yanajenga msingi wa Mageuzi ya Chama chetu lazima yashirikishe wanachama wetu.

CCM kama chama cha siasa ili kifanye kazi yake vizuri na yenye matokeo makubwa chanya, ilikusudiwa lazima kihuishwe ili kiweze kwenda na wakati na kutekeleza matakwa ya wanachama, kwa kuzingatia ukweli kuwa lengo kuu la chama chochote cha siasa ni kushika dola.

Mabadiliko ya Kikatiba ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yana lengo la kukiimarisha chama chetu ili kuziteka hisia, mioyo na fikra za watanzania wengi, kwa nia ya kukiunga mkono katika lengo lake la kushika dola na kuleta maendeleo endelevu kwa watanzania.

Katiba ya CCM imekuwa ikifanyiwa marekebisho mara kwa mara tangu ilipotungwa mwaka 1977, kwa madhumuni ya kuiboresha ili iendane na wakati uliopo. Kwasababu hiyo, yamekuwepo matoleo 12 ya Katiba hii hadi mwaka 2012. Katiba ambayo imepitishwa na Mkutano Mkuu Maalum tarehe 12 Machi 2017 jijini Dodoma, inakuwa toleo la 14.

Mabadiliko haya yanalenga kurekebisha Muundo, Mfumo, Uongozi, Utendaji na mengineyo.

Mambo muhimu ambayo yamezingatiwa katika marekebisho haya ni yafuatayo; -  ITAENDELEA KESHO

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top