0
Katibu mkuu wa balaza la Sanaa la Taifa BASATA Godfrey Mngereza ametoa taarifa za kuufungia wimbo wa msanii wa nyimbo za bongo freva Nay wa Mitego aliyetoa wimbo mpya uliobeba jina la ‘WAPO’ kuwa hauna maadili.


DAR ES SALAAM.
Katika taarifa yake amesema wimbo huo unavipengele vinavyochochea vurugu pia hauna maadili kwa jamii ya watanzania lakini pia sheria inachukua mkondo wake, ameongeza kuwa kukamatwa kwa Nay hakutokani na wao Basata tu, maana sheria inagusa sehemu nyingi kwani Basata ni serikali na hata waliomkamata ni serikali pia.

Aitha amesema maamuzi wanayochukua ni kuzuia wimbo amabo hauna maaadili hata radio.“anayekamatwa na ngozi ndiye mwizi, kwani katika utangazaji kuna (ethics) kanuni zake , hivyo nikisikia kituo kinaupiga basi atakayepatikana kuupiga  nayeye atahusika katika sheria, kazi ambayo inatukana watu, inachochea vurugu hata kama hujamtaja mtu jina moja kwa moja, inavunja sheria na maadili nitashangaa kusikia kazi chafu inapigwa na mtu mzima mwenye akili timamu tena anasikiliza, sasa kutokana na hilo unajenga kizazi cha namna gani ?” alisema Godfrey Mngereza.

Hapa nchini sheria kwa kuanzia na sheria mama ambayo ni katiba ya nchi zipo na zinazuia mtu kutukana adharani au vitu visivyo na maadili ya mtanzania, hivyo basi mkono wa sheria ni mrefu unaweza kukuchukua pale wanapoona unafanya makosa ya kuvunja sheria za nchi.


Hata hivyo kutokana si mara ya kwanza kwa Nay kukamatwa kutokana na makosa tofauti yakiwemo ya kutoa nyombo zisizoendana na maadili ya kitanzania hali hii itapelekea kupewa adhabu ambayo BASATA watakaa na kushauliana na wanasheria ili kuona hatua gani stahiki watamchukulia.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top