0
Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya ISTEP yaendesha warsha ya mafunzo katika nyanja ya mazingira, masoko pamoja na kuwezesha wataalam walio katika sekta ya elimu kupitia wakufunzi kutoka vyuo vya ufundi nchini kuangazia utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati mbadala ili kuweza kupunguza uchafuzi wa mazingira.
Warsha hiyo inayofanyika kwa siku tatu jijini Arusha imewakutanisha wadau na wakufunzi kutoka mikoa kadhaa nchini na wadau wengine kutoka Taasisi ya vyuo Canada (CICan), Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (MOEST) na Serikali ya Canada kwa pamoja wanaendesha warsha hiyo ikiwa ni sehemu ya kuendeleza mazingira na kukabiliana na Tabia nchi.
Hapa chini tunakuletea baadhi ya matukio katika picha ambayo yamejiri wakati wa warsha hiyo inayofanyika katika Hotel ya VETA Njiro jijini Arusha.

ARUSHA.
Assela Marcellus Luena aliyekaa ameshika kipaza sauti kutoka Balaza la Taifa la elimu ya Ufundi (NACTE) akichangia mada kuhusu madhara yatokanayo na matumizi ya vifaa vya kisasa, pembeni ni Dr. Alan Copeland akimsikiliza.


Dr, Alan Copeland (aliyesimama kashika kiuno) ni Mtaalam mwandamizi wa ufundi kutoka I STEP Tanzania, akisimamia mada inayohusu mazingira endelevu na nafasi ya zana kwa taasisi, idara na wizara.
Akichangia mada ya faida, hasara zitokanazo na matumizi ya Solar na Genereta, Dr. John Msumba (kulia) kutoka Taasisi ya Teknolojia na Ufundi (DIT) kushoto ni Dr Alan Copeland wakiangaliana.




Mkuu wa chuo cha VETA mikumi Christop Jacob Ayo (wanne kutoka kulia) akielezea faida wanazopata kutokana na matumizi ya umeme jua wanaotumia ikiwa ni pamoja utunzaji wa mazingira ili kuiweka dunia katika ukijani, wengine kutoka kushoto ni Afridon Mkhomoi, Romana, kulia ni Michael Hey, Charles Mpambwe na John Kengese wote. 

Dr. John Msumba kutoka Taasisi ya Teknolojia na Ufundi (DIT) akifafanua umuhimu wa kutumia nishati ya jua katika matumizi mbalimbali ili kuepukana na garama zinazoweza kuepukika.


Wakiteta jambo la furaha kulia ni Happiness Salema, mama Mbwambo na Leah Lukindo wakati mapumziko mafupi.
Baada ya ufunguzi wa warsha iliyokusanya wataalam na wakufunzi wa elimu kutoka vyuo kadhaa nchini vya VETA pamoja na biashara wakiwa katika picha ya ukumbusho katika hotel ya VETA Njiro jijini Arusha.

PICHA NA: Todays Production
+255 757 800 307  




ARUSHA.
Warsha hiyo inayofanyika kwa siku tatu jijini Arusha imewakutanisha wadau na wakufunzi kutoka mikoa kadhaa nchini na wadau wengine kutoka Taasisi ya vyuo Canada (CICan), Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (MOEST) na Serikali ya Canada kwa pamoja wanaendesha warsha hiyo ikiwa ni sehemu ya kuendeleza mazingira na kukabiliana na Tabia nchi.

Wakati nchi ikiwa katika mchakamchaka wa maendeleo kwenda kwenye uchumi wa viwanda ambapo pasipo utunzaji wa mazingira ni vigumu kufikia hatua inayotakiwa, wakati moja ya ajenda inayojadiliwa katika warsha hiyo ni utunzaji wa Mazingira, likiwepo suala la Maji pamoja na Nishati.

Leah Mkimbo ni mkurugenzi wa mafunzo VETA anasema “sisi kama watoa mafunzo suala la mazingira tunalipa kipaumbele sana, na lipo katika mitaala yetu ambapo kupitia ushirikiano na vyuo vya Canada, wanatujengea uwezo kutokana nafasi yao kuwa wanafanya vizuri kwa upande huo, ukiona mwenzako anafanya vizuri, usikae mwenyewe bali jifunze kutoka kwake”.


Leah Mkimbo Mkurugenzi wa mafunzo VETA 
Pamoja na mazingira kuwa na mjadara mkubwa hivi sasa duniani warsha hiyo pia imeweza kuwapa fulsa wadau, waalimu na wataalam waliohudhulia kujadiri suala la Maji, “maji ni malighafi muhimu sana katika maendeleo ya mwandamu, ikiwa unazungumzia viwanda au maendeleo ya watu kiuchumi, hivyo tunapaswa kuboresha miundombimu ya maji na kutoyapoteza maana maji yanapotea kwa wingi sana katika majumba yetu” anasema Leah Mkimbo.


Wakati maji yanayotoka katika mfumo wa maji taka wa majumbani yanaweza kufanyiwa mpangilio mzuri na kurejea katika matumizi mengine kama kwenye bustani hama hata katika matumizi ya ndani, hivyo basi mifumo kama hiyo ndiyo inapaswa kuingizwa katika mitaala ili wanafunzi wanaomaliza na kurudi mtaani waweze kuwafundisha wananchi namna ya kutumia hii mifumo.

Nishati ni kitu muhimu katika maendeleo yoyote hasa katika uchumi wa Viwanda, na garama ya nishati inayotumika ni kubwa sana, wakati umeme unaotumika nchini unatokana na maji na kuna baadhi ya wananchi hawapati huduma hiyo hivyo nishati mbadala inayotokana na jua, upepo na takataka ambapo umeme wake unawezaz kutumika sehemu yoyote na kwa garama nafuu baada ya kufunga vifaa vinavyohitajika.
  
Afridon Mkomoi -VETA Shinyanga.
“Mitambo ya migodini na inayotumika katika mashamba ni sehemu ya mfunzo tunayopata katika warsha hii, kutokana na sisi kama watumiaji wa mitambo ni lazima tuwe na elimu ya kutunza mazingira, usipotunza mazingira wananchi wanahathirika, mpaka hapa tunaenda kuandaa mtaala ambapo jamii inapokuwa na mahitaji ya utunzaji wa mazingira watakuja kwetu na kupata kile wanachokitaka kuhusu utunzaji mazingira” anasema Afridon Mkomoi mkuu wa VETA Shinyanga.


Hata hivyo changamoto ni kubwa katika nchi zinazoendelea kutokana na uharibifu wa mazingira unaosababisha mabadiriko ya tabia nchi, hali hii inaweza kuleta tija endapo taasisi zinazotoa mafunzo ziwawezeshe wale wanaopewa mafunzo kwa kiasi kikubwa ili waweze kutoa elimu kwa mifano itakayozaa matunda na baadaye mafunzo watakayopewa wananchi wanaozunguka eneo husika waone kupitia kile mtoa mafunzo ananchomaanisha.


Post a Comment

 
Top