0
Mwezi Novemba mwaka uliopita, alizuiwa jijini Nairobi nchini Kenya wakati anajiandaa kubadili ndege kwenda jijini Kigali, baada ya serikali ya Rwanda kuitaka Kenya kutomruhusu kufika Kigali.
PHOTO: Kiongozi wa Upinzani anayeishi nchini Ufaransa Thomas Nahimana.
Reuters.
Hali ya sintofahamu imeripotiwa nchini Rwanda baada ya kasisi wa zamani ambaye kwa sasa ni kiongozi wa upinzani nchini humo Thomas Nahimana, kutangaza kuunda serikali sambamba na utawala uliopo madarakani wa Rais Paul Kagame.
Thomas Nahimana amechukuwa uamuzi huo baada ya kupigwa marufuku kuingia nchini humo kujiandikisha kama mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi mkuu unaopangwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu.
Kiongozi uyo wa upinzani ambaye kwa sasa yupo uhamishoninchini Ufaransa anasema lengo la serikali yake ni kuiondoa madarakani serikali ya Rais Paul Kagame, wakati Thomas Nahimana amekuwa akiushutumu utawala wa Paul Kagame ya kwamba unavunja sheria na kukandamiza wananchi.
Mwanasiasa huyo ambaye anatumia pasi ya kusafiria ya Ufaransa, tayari ametangaza nia ya kuwania urais nchini humo mwezi Agosti mwaka huu, hata hivyo hivi karibu alitarajiwa kurejea nchini Rwanda akitokea jijini Brussels nchini Ubelgiji, lakini hakuweza kufanya hivyo baada ya kudai kuwa serikali ya Kigali inaendelea kumwekea vikwazo.
Yves Butera, msemaji wa Idara ya Uhamiaji nchini Rwanda wakati huo alisema kuwa Padri huyo atakaribishwa nchini Rwanda kama raia mwingine, hata hivyo kiongozi huyo wa upanzini Thomas Nahimana amesema kuwa serikali yake itakua ikifanya kazi ikiwa uhamishoni.


Fist appeared from rfi

Post a Comment

 
Top