0
Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) pamoja na Kampuni ya Sunshine Group Ltd ya nchini China kwa pamoja zimeingia mkataba wa makubaliano wa miaka mitano ya kushirikiana katika kuratibu  na kufadhili  miradi ya elimu katika mikoa mbalimbali hapa nchini.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania, Graceana Shirima (kushoto),  akizungumza  na waandishi wa habari katika hafla ya kusaini makubaliano ya miaka mitano ya kusaidi a miradi ya Elimu,  kulia ni  Mkurugenzi Mtendaji wa, Sunshine Group Ltd, Tony Sun.



DAR ES SALAAM
Na John Simon Luhende
Makubaliano hayo  yametiwa saini na kaimu mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania bibi Graceana Shirima na mkurugenzi na mkurugenzi wa kampuni ya Sunshine Group Ltd  bwana Tony Sun Tao leo tarehe 20/2 /2017  katika ofisi za Mamlaka hiyo jijini Dares salaam.

Akizunguza na waandishi wa habari wakati wa kusainin makubalianao hayo Kaimu mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania bi Graceana Shirima  amesema  makubalianao hayo yanawezesha  kampuni ya Sun shine kufadhili miradi mbalimbali katika sector ya  Elimu, hivyo basi kupitia makubalianao hayo TEA itakuwa mratibu mkuu na Sunshine wao watakuwa wakifadhili tu.

Aidha bi shirima amewashukuru TEA na uongozi wa Sunshine kwa kuona umuhimuwa kushirikiana katika kutekeleza  miradi ya Elimu nchini, na kusemakuwa katika kutekeleza miradi hii watashirikiana na  Wizara pamoja na  Halmashauri.

“Napenda niwahakikishie kuwa tutaratibu vizuri miradi yote katika muda wote wa miaka mitano ya makubaliano haya na mamlaka itawatunukia  hati ya utambuzi (CEA) kwa ajili ya kutambua mchango wenu katika sekta hii ya Elimu” alisema Bi shirima.

Naye Mkurugenzi wa kammpuni ya Sunshine Goup Ltd Bwana Tony Sun miradi ya kwanza kutekelezwa  kupitia makubaliano hayo kuwa ni  ujenzi wa maabara mbili za sayansi katika shule ya sekondari Matundasi  iliyoko katika Wilaya ya Chunya  mkoani Mbeya  na kujengea madarasa na miundombinu  ya Maji  katika shule ya Sekondari Bunda iliyopo mkoani Mara na kuongeza kuwa miradi hiyo itagharimu jumla ya apesa za kitanzania  million 210.

“Tutafadhili kwanza katika mikoa na maeneo ambayo tunafanya shughulizetu katika mikoa ya Dar es salaam, Mwanza, Dodoma, Mbeya,Mara na Mtwara”. Alisema mkurugenzi huyo

Post a Comment

 
Top