0
Tamasha linalotoa nafasi kwa wananchi na wanafunzi mbalimbali kujifunza na kupata fulsa ya kuibua vipaji kuviendeleza, Kufaham Tanzania na vivutio vyake hasa vilivyo kusini, watoto kupata nafasi ya kujifunza kuchora katuni na pamoja namaonyesho ya biashara linatarajia kufanyika mkoani Songea hivi karibuni.

Muandaaji mkuu wa Tamasha la Majimaji Selebuka Reinafrida Rwezaura akiongea na wanahabari (hawapo pichani) juu ya tamasha kubwa kwa mkoa wa Ruvuma.


Mshindi wa pili wa mbio za baiskeli km 100 Allen Nyanginywa (kulia) akiongea juu ya nafasi aliyopata ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya baiskeli nchini Afrika kusini katikati ni Reinafrida Rwezaura na kulia ni Muandaaji msaidi wa Tamasha hilo Merania Luoga.


Muandaaji mkuu wa Tamasha la Majimaji Serebuka Reinafrida Rwezaura akionyesha tiketi tatu za washindi wanaotarajia kuondoka hivi karibuni kuelekea nchini Afrika kusini.
Reinafrida Rwezaura akimkabidhi tiketi tatu Allen Nyanginywa kwa ajili yake na  washindi wenzake wawili (ambao hawakuwepo) ili kuelekea Afrika kusini kushiriki mashindano.


DAR ES SALAAM.
Tamasha hilo linalojulikana kama MAJIMAJI SELEBUKA linatarajiwa kufanyika mwaka jana lilifanyika mwaka jana 2016 mwezi wa Octoba na msimu wa pili kufanyika mwezi Mei 28 hadi 04June 2016 hivyo kupelekea kufanyika kwa mwaka huu tarehe 23 hadi 30 Julai 2017, ambapo washindi wa mbio za baiskeli kilomita 100 wanatarajiwa kwenda nchini kushiriki mashindano ya baiskkeli mwaka 2018.

Akizungumza katika mkutano wa wanahabari muandaaji mkuu wa Tamasha hilo Reinafrida Rwezaura amesema kuwa “pamoja na nafasi mbalimbali kama fulsa ya  Kupanua soko kwa wajasiliamali, wafanyabiashara na wanafunzi kupitia midaharo katika shule za Sekondari kwa wakazi na majirani kwa mkoa wa Ruvuma pia watapata zawadi kutokana na kushiriki mashindano ya marathoni ya kilomita 42 ambapo mshindi wa kwanza atapata Tsh 1,500,000, wa pili 1,000,000 na watatu atapata 500,000”.
Vilevile mshindi wa pili wa mashindano ya baiskeli kwa kilomita 100 kutoka mbinga kuelekea Songea Allen Nyanginywa amekabidhiwa tiketi tatu kwa niaba ya mshindi wa kwanza Salum Miraji na mshindi wa tatu Ipyana Mbogela ambao hawakuwepo kwa ajilin ya safari ya kuelekea katika mji wa Johannesburg nchini Afrika kusini kushiriki mashindano ya Chem ride for sight 2017.


Post a Comment

 
Top