Maharusi waliowasisimua watu wengi baada ya kutumia kiasi cha Sh100 pekee za Kenya kugharimia harusi yao, hivi karibuni waliandaliwa sherehe kubwa ya harusi ambayo imeafanyika hapo jana katikati ya viunga vya jiji la Nairobi.
![]() |
| Haki miliki ya picha AALTONEN JUMBAI Harusi ya marudio ya Wilson na Anne imeandaliwa katika bustani ya kifahari. |
Sherehe
hiyo ya marudio imeandaliwa katika bustani ya Eden Bliss ambayo ni bustani ya kifahari iliyopo viungani mwa Nairobi na imeashimishwa hapo jana wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Wapendanao.
Harusi
ya awali ya Anne na Wilson Mutura iligharimu dola moja pekee ya Kimarekani
lakini sherehe ya sasa inakadiriwa kwamba imegharimu takribani Ksh 3.5 milioni
(zaidi ya Tsh 70milioni).
Pesa hizo zimegharimiwa na makundi mbalimbali yanayohusika
katika uandaaji wa sherehe, ambayo yaliungana kwa pamoja na kuchanga pesa
kuwaandalia Anne na Wilson sherehe hiyo ya kukata na shoka.
Mmoja
wa waandalizi wakuu wa harusi hiyo Aaltonen Jumba kutoka Slique Events Planner
Limited, anasema ni vigumu kujua hasa ni kiasi gani cha peza zilitumiwa
kuiandaa.
Pamoja na kwamba wahudumu mbalimbali walijitokeza kusaidia kutoa huduma zao, ila hakuna pesa taslimu zilizotolewa. Lakini kuna
waliotoa mahema, wengine viti, wengine magari ya kifahari.
![]() |
| Wawili hao wamesafirishwa kwa magari ya kifahari |
Kwa sababu walikuwa tayari washafunga ndoa rasmi, kwenye sherehe ya leo, walibadilisha pete zao. Baadhi ya Wakenya mitandaoni wamekuwa wakikosoa uamuzi wa kutumia pesa nyingi kugharimia sherehe nyingine ya harusi kwa wawili hao. Lakini Bw Jumba anasema wanaokosa sherehe hiyo wamekosa kutambua na kufahamu vyema mambo ambayo yamekuwa yakijiri.
"Wawili hao tayari wamesaidiwa kifedha. Wamepewa shamba la
kisasa, wakalipiwa fungate na wameahidiwa pesa za kutumia kama mtaji kuanzisha
biashara, kwa sababu yote yameshughulikiwa, kwa nini tusiwape kile
ambacho walikosa? Kila mtu hutamania sana kuwa na sherehe kubwa ya
harusi."
![]() |
| Haki miliki ya picha NDUNGU NYORO / FACEBOOKI Bw Wilson akisaidiwa kuweka sawa koti lake |
![]() |
| Haki miliki ya picha NDUNGU NYORO / FACEBOOK Bi Anne wakati wa sherehe ya harusi ya marudio |
Wawili hao, wanaoishi eneo la Kasarani, Nairobi, walisifiwa kwa kuonyesha thamani halisi ya mapenzi badala ya kuongozwa na pesa.
Zaidi ya kuandaliwa harusi hiyo, wametunukiwa shamba la kilimo cha kisasa, fungate
kwenye hoteli ya kifahari na baada ya sherehe ya leo wanatarajiwa kwenda kwa
fungate nyingine mjini Dubai.
Dola
yenyewe walioyotumia Anne na Wilson katika harusi yao ya mwanzo waliitumia
kununua pete mbili. Walikuwa
wameahirisha harusi yao mara tatu baada ya kukosa fedha za kutosha kuandaa
sherehe kubwa ya harusi. Maombi
yao kwa familia na marafiki kuwafanyia mchango, hayakutimizwa.
Baada
ya muda, Bwana harusi, Wilson, hakuwa na la kufanya ila kumshawishi mpenzi wake
kuhusu uwezo wake. "Wilson
aliponieleza hali yake, sikukataa. Mapenzi yetu yalizidi yote," anasema Anne
Ingawa
walikuwa na uwezo wa kuishi kwa mtindo wa 'come we stay' uliomaarufu kwa vijana
wengi ambapo wapenzi wanaishi pamoja bila kuoana, Wawili hao walikwenda kwa
askofu Jasper Owach kutoka Kanisa la Community Christian worship centre mjini
Nairobi kurasmisha harusi yao.
"Mapenzi
yetu yalidumu kwa muda na ili kujisitiri kutoka maovu baada ya kupata baraka ya
wazazi, tuliamua kufanya mambo yetu rasmi," anasema Wilson.
![]() |
| Wilson Muturi na mkewe Ann walitumia dola moja pekee wakati wa harusi yao |
Siku yenyewe ilipofika, bwana Harusi, Wilson aliwashangaza waumini baada ya kukimbia nje sherehe ikiendelea. "Alitoka ghafla kununua pete ya harusi nilipokuwa naendelea na shughuli ya kuwafunganisha," alisema askofu Jasper Owach, ambaye aliongoza hafla hiyo.
Wilson
alirejea na walipokuwa wanatamka kauli za ndoa, Wilson alitoa pete hizo
zilizofungwa kwa gazeti na wakavikana pete. Wawili
hao, wamewapa hamasa vijana kutozuiwa na uwezo wao wa kifedha na hivyo basi
kuhalalisha mapenzi yao kupitia ndoa.
This story is from & appeared firstly on bbcswahili.





Post a Comment