0
Takribani watanzania wapatao 132 wanaoishi nchini Msumbiji wamefukuzwa nchini humo huku wengine wasiojulikana wakidaiwa kukamatwa kufuatia operesheni iliyoanzishwa na serikali ya nchi hiyo hivi karibuni.

Sehemu ya mji Monte Puez nchini Msumbuji ambao ni maarufu kwa uchimaji wa madini.
Kulingana na taarifa ya serikali ya Msumbiji inasema operesheni hiyo inalenga kuwatimua raia wa kigeni wanaoishi nchini humo kinyume cha sheria.
Kwa upande wa taarifa ya wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki nchini Tanzania imesema kuwa raia waliofukuzwa ama kukamatwa ni wale wanaoishi mji wa Monte Puez kwa kuwa una raia wengi wa kigeni ikilinganishwa na miji mingine.
Kutokana na taarifa hiyo tayari ubalozi wa Tanzania nchini Msumbiji unaendelea kufanya mawasiliano ya kidiplomasia na serikali ya Msumbiji ili kuwahakikishia usalama raia wa Tanzania na mali yao nchini humo upo salama
Inakadiriwa kuwa, Watanzania wapatao elfu tatu (3,000) wanaishi na kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii katika mji huo wa Monte Puez, ambapo hatua hiyo inakuja licha ya mataifa ya Msumbiji na Tanzania kufanya mkutano wa kuainisha maeneo ya ushirikiano yakiwemo maswala ya kibiashara na uhamiaji.
Huku operesheni hiyo ikiendelea hivi karibuni serikali imekuwakumbusha Watanzania wote waishio ughaibuni, kufuata Sheria na taratibu za nchi hizo wanazoishi ili kuepukana na madhara yoyote yanayoweza kujitokeza pindi wananapokuwepo katika nchi hizo.
                                                                                         

Firstly appeared in bbcswahili.

Post a Comment

 
Top