0
Kila raia ana tashwishwi ya kupata haki pale panapokuwepo na hitaji litokanalo na uwepo wa sheria pindi sheria inapovunjwa au kupindishwa kutokana na makossa ikiwa na maana pasipo makosa basi hakuhitajiki sheria maana itakuwa butu pasi  kutumika.


Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Arusha Sekera Mosho akitoa hotuba wakati wa maadhimisho hayo mapema leo jijini Arusha.


Meya wa jiji la Arusha Lazaro Karisti kushoto akiteta jambo na Jaji mstaafu (….) kulia na wengine ni majaji wa mahakama kuu  wakati wakielekea katika viwanja vya maadhimisho ya siku ya Sheria.

Mahakimu na wanasheria wa mkoa wa Arusha wakiwa katika maandamano kuelekea eneo la sherehe ya siku ya Sheria nchini.

Mazoezi ya mwili ni muhimu ili kuuweka mwili katika muonekano na afya njema, kijana huyu ambaye jina lake halaikuweza kupatiukana aliweza kuwaonyesha wanasheria kuwa mwili ukiupatia mazoezi unaweza kuukunja vile unataka.

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo wa nne kulia akiwa na Majaji wa mahakama kuu wenye majoho mekundu na wengine waliosimama ni wanasheria na mawakili, Kamanda wa jeshi la polisi  kulia aliyesimama na jeshi la magereza wanne kushoto waliosimama pamoja na majaji katika picha ya pamoja, akiwepo meya wa jiji la Arusha (kulia aliyekaa).


ARUSHA.
Wanasheria nchini wameadhimisha siku ya sheria ikiwa ikiwa a kauli mbiu “Umuhimu wa utoaji haki kwa wakati kuwezesha ukuaji wa uchumi” ambapo mkoan Arusha sherehe hizo zimefanyika katika viwanja vya mahakama kuu ya kanda ya Arusha na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali.

Akitoa hotuba ya chama cha mawakili Tanganyika kanda Arusha, Mwenyekiti wa chama cha mawakili wa kujitegemea kanda ya Arusha Modest Akida amesema, maudhui ya kauli mbiu ya mwaka huu yamelenga kwenye msukumo wa serikali ya awamu ya tana wa kujenga uchumi, ikiwa na maana pamoja na mambo mengine, biashara na uwekezaji.

“ukuaji wa biashara na ongezeko la uwekezaji huenda sambamba na mfumo wa utoaji haki katika nchi ambapo kazi kuu ya mfumo huo ni kulinda haki pale migogoro inapotokea alisema Modest Akida, Mwenyekiti wa mawakili wa kujitegenmea.

Wakati haki ni neno lililozoeleka midomoni pamoja na masikioni mwa watanzania, wakati huo huo kila uchao watoto, vijana, wanawake, wanaume, wazee, kina mama, wafanyakazi, waajili kwa ujumla siku haipiti miongomi mwao kusikia wakidai haki. Neno hilo ‘haki’ ni dhana pana inayohusisha mamlaka mtambuka.


Post a Comment

 
Top