![]() |
| PHOTO PROFILE: Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza. |
ARUSHA.
Serikali ya Burundi imetoa tamko jana Jumatano kwamba
haitapeleka ujumbe wake katika mazungumzo ya upatanisho yanayoendelea jijini Arusha, Tanzania.
Mazungumzo hayo yanayolenga juu ya kutafuta ufumbuzi
wa mgogoro wa kisiasa nchini Burundi yalitarajiwa kuanza leo Alhamisi, lakini
kuna wasiwasi ulioendelea kwamba mazungumzo hayo hayatasaidia kuleta amani
katika nchi hiyo ya Afrika ya Kati inayokabiliwa na mgogoro wa kisiasa.
Wapinzani na asasi za kiraia wanasema msimamizi wa mazungumzo hayo, rais mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa, anavuruga mchakato huo kwa kuwakaribisha wanasiasa ambao walifanya jaribio la kumpindua Rais Pierre Nkurunziza mwaka 2015.
Wapinzani na asasi za kiraia wanasema msimamizi wa mazungumzo hayo, rais mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa, anavuruga mchakato huo kwa kuwakaribisha wanasiasa ambao walifanya jaribio la kumpindua Rais Pierre Nkurunziza mwaka 2015.
Appeared first in VOA Swahili.

Post a Comment