0
Chama cha wananchi CUF kikiwa katika msuguano wa kiuongozi na Prof. Ibrahim Lipumba kutokana na msigano wa kiuongozi, chama hicho leo kupitia mkutano mkuu wa tawi la Chanjaani, Jimbo la mkoani wilaya ya Mkoani-Pemba kimefanya maamuzi ya kumfukuza uanachama wa CUF ili aweze kuendelea na majukumu yake mtaani  Mohamed Habibu Mnyaa.


Profile PHOTO:  Mohamed Habibu Mnyaa. 


MKOANI PEMBA.
Fukuza hiyo imetokana na Mohamed Mnyaa kwenda kinyume na kukiuka katiba ya chama hicho kwenye Ibara ya 12 (6)(7)(16) ambapo inasemekana amekuwa na mienend isiyofaa inayopelekea kuwagawa wanachama, kueneza taarifa za upotoshaji dhidi ya viongozi na Chama, pia vitendo vya hujuma za kutaka kukidhoofisha Chama, kudharau na kushindwa kuhudhuria pamoja na kushinwa kutoa ushirikiano kwa tawi lake pale alipotakiwa kufanya hivyo.

Akitoa maamuzi hayo katibu wa tawi la Chaanjani jimbo la mkpani Pemba Kombo mohamed maalim amesema mkutano wetu mkuu wa leo umehudhuriwa na wajumbe halali 112 kati ya wajumbe wote halali 113, hivyo wajumbe wote 112 wamepiga kura za ndio kuazimia kumfukuza uanachama kwa mujibu na mamlaka ya kikatiba yaliyoelezwa katika katiba ya CUF uliopo ukurasa wa 29 ibara ya 18 kifungu (1)(ix) kuhusu wajibu wa mkutano Mkuu wa Tawi kama ilivyoeleza;

 “Kumchukulia hatua za nidhamu mwanachama au kiongozi yeyote wa tawi, ikiwa ni pamoja na kumpa onyo, karipio, karipio kali, kumsimamisha uanachama au uongozi wa Chama kwa muda, na hata kumuachisha au kumfukuza uanachama wa Chama” 


Mohamed Habibu Mnyaa ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo la Mkanyageni kwa vipindi viwili 2005 mpaka 2015 alijiunga na CUF katika tawi hilo tarehe 28 septemba mwaka 1999 ambapo alikabidhiwa kadi yenye namba 029033. Maalim ameongeza kuwa mwenendo huo mbaya na usiofaa kwa Chama na viongozi wake tangu alipokosa ridhaa ya wanachama na Maamuzi ya vikao vya Chama kumpitisha kugombea kwa mara nyingine tena katika nafasi ya ubunge mwezi August, mwaka 2015. 

Maalim alisema “Tunatoa wito kwa wanachama wote wa tawi la Chanjaani, kuzingatia wajibu wao wa kikatiba na kuheshimu taratibu, kanuni na kulinda nidhamu na heshima ya Chama chetu ndani ya Chama na ndani ya jamii kwa ujumla. Uongozi wa tawi hautasita kutekeleza matakwa ya katiba pale itakapobainika kwa mwanachama yeyote kwenda kinyume na maamuzi na misimamo ya Chama”






Kombo mohamed maalim

Katibu wa tawi la chanjaani, jimbo la mkoani-pemba Imetolewa leo Tarehe 7/2/2017

Post a Comment

 
Top