0
PHOTO PROFILE: Mfano wa madhara yatokanayo na tetemeko la aridhi.

























Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.7 kwenye vipimo vya Richter limeikumba eneo la ziwa Tanganyika majira ya saa tisa na dakika thelathini na mbili usiku kuamkia leo, tetemeko hilo lilitikisa maeneo ya kaskazini mwa Zambia na mitetemo yake kufika maeneo ya kusini magharibi mwa mwa mkoa wa Rukwa.

Kwa mujibu wa shirika la Utafiti wa Jiolojia la nchini Marekani linasema kitovu chake kilikuwa kilomita 10 chini ya ardhi, umbali wa takribani kilomita 45 mashariki mwa mji wa Kaputa nchini Zambia, mji huo unapatikana katika mpaka wa Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa kama huo huchukuliwa kuwa la kawaida, lakini wataalamu wanasema kutokana na kitovu chake kuwa chini sana ndani ya ardhi, huenda hilo lilisababisha mtikisiko kuwa mikubwa.



Jiolojia image: Jinsi tetemeko linavyoanza chini ya ardhi.




Source: bbc swahili

Post a Comment

 
Top