0


Tunakuletea habari zaidi juu ya safari hii iliyomfikisha hapa nchini waziri wa mambo ya nje wa china Mh. Wang Yi aliyepokelewa na mwenyeji Mh. Dr Augustine Maiga kisha kwenda kuonana na Waziri mkuu Kassim Majaliwa na baadaye kulekea katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwl Nyerere jijini Dar Es Salaam -JNICC.


.



Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akiongea jambo na mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Wang Yi ofisi Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam na kukubaliana kuendelea kuimarisha zaidi mahusiano kati ya Tanzania na China.Kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga.


Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akiongea jambo na mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Wang Yi ofisi Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam na kukubaliana kuendelea kuimarisha zaidi mahusiano kati ya Tanzania na China.Kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga.


Waziri wa mambo ya nje wa china Wanag Yi mwenye Tie ya blue bahari akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwl nyerere kuongea na wanahabari juu ya ziara yake hapa nchini.

Akiongea na mwenyeji wake Mh, Dr. Augustine Maiga ambaye ni waziri wa mambo ya nje, kikanda na kimataifa.

Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi akisaini kitabu caha wageni kuweka kumbukumbu kwamba aliwahi kufika hapa nchini.

Mh. Dr Augustine Maiga wa pili kulia akongea na mgeni wake hayupo pichani juu ya mpango wa serikali wa kuhamia Dodoma.

Mh. Wang Yi mbele katikati akiongea na mwenyeji wake waziri Maiga (hayupo pichani) juu ya serikali ya China ilivyo na mipango kadhaa juu ya Tanzania.

Mara baada ya mazungumzo mafupi walishikana mikono kuashilia kuendelea kushirikiana katika nyanja kadhaa za maendeleo hususani katika ujenzi wa viwanda hapa nchini.

Balozi Augustine Maiga kulia pamoja na waziri wa mambo ya nje wa china Wang Yi kushoto wakiongea na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu uwekezaji unaokwenda kufanyika kupitia viwanda hapa nchini.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>...

Post a Comment

 
Top