Robin
Rhodes mwenye umri wa miaka 57 anatuhumiwa kwa kusema Trump .... atawafukuza
nyinyi nyote na baadaye akamzuia mwanamke huyo kutoondoka katika afisi yake.
![]() |
| Profile Photo: Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa John F. Kendedy. |
MAREKANI.
Robin Rhodes mwenye umri wa
miaka 57 anatuhumiwa kwa kusema Trump ....atawafukuza nyinyi nyote na baadaye
akamzuia mwanamke huyo kutoondoka katika afisi yake.
Kushambulia na kuwazuilia watu
ni miongoni mwa mashtaka ya uhalifu wa chuki ambao mtu huyo kwa sasa
anakabiliwa nayo, pia atakabiliwa na kifungo cha miaka 4 jela iwapo atapatikana
na hatia kulingana na hakimu wa mahakama katika Wilaya ya Queens, Pia
ameshtakiwa kwa kupiga kelele.
Mfanyakazi huyo wa kampuni ya ndege ya Delta Airlines
ambaye alikuwa amevaa hijab alikuwa ameketi katika afisi yake siku ya Jumatano
wakati Rhodes alipodaiwa kwenda katika mlango wake na kuanza kumkaripia,
kugonga mlango, kumzuia kuondoka na kumpiga teke.
Wakati mtu mwengine
alipoingilia kati na kumsaidia mwanamke huyo kutoka ofisini kwake, mtu huyo
alidaiwa kumfuata na kupiga magoti mbele yake akiigiza maombi ya kiislamu. ''Islam na Isis, sasa Trump amewasili,
atawafurusha nyotea, unaweza kuuliza Ujerumani, Ubelgiji na Ufaransa kuhusu
watu hao utaona kilichojiri''.
Source BBC

Post a Comment