Tamasha
la utalii na kupiga vita ujangiri, tembelea mbuga zetu limekusanya jumuiya za
waandishi pamoja na wadau wa sekta ya utalii katika jiji la
Arusha huku kukiwepo na mada mbalimbali zinazogusia changamoto za utalii,
sheria za kiuandishi, ujangiri pamoja na uandishi wa habari za utalii ambapo
tamasha hilo limeanza kwa kuwepo kwa mijadara kadhaa.
![]() |
Katibu wa vyama vya waongoza watalii nchini Emmanuel Mollel
azungumzia changamaoto kadhaa zinazowakabili kwa upande wao.
|
![]() |
| Wadau wa sekta ya utalii na wana habari wakifuatilia majadiliano wakati wa Arusha Tourism Festival (conference) iliyofanyika mapema leo jijini Arusha |
![]() |
Loshee Mollel kiongozi wa wapagazi akizungumza juu ya kazi
wanazozifanya wasaidizi wa watalii wawapo katika kazi zao.
|
![]() |
Afisa utalii wa mkoa wa Arusha Flora akielezea namna
serikali inavyowakilishwa katika jamii ambapo raia yeyote ana nafasi katika
maendeleo ya nchi, kulia kwake ni wadau wa sekta ya utalii.
|
![]() |
Waandishi wa habari na wadau wakiwa katika picha ya kundi
wakati wa mijadara ya tamasaha la utalii na wana habari jijini Arusha.
|
![]() |
Waandishi wa habari na wadau wa sekta ya utalii wakiwa
katika mkutano wa mijadala kuelekea kwenye Tamasha la Utalii Arusha.
|
![]() |
Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri mkoani Arusha Claudi John
akitoa mchango kuhusu changamoto za sekta ya utalii pamoja na waandishi wa
habari.
|
![]() |
Neville
Meena mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini akitoa semina kwa wadau wa utalii
na waandishi wa habari katika hoteli ya Palace Hotel.
|
ARUSHA.
Wakizungumza
katika majadiliano yaliyofanyika siku moja kabla ya tamasha litakalofanyika
kesho katika uwanja wa sheikh Amri Abeid jijini Arusha katibu
wa vyama vya waongoza watalii nchini Emmanuel Mollel amesema waongoza watalii wanapata
wana changamoto zinazowakabili zikiwemo kuhitaji, marekebisho ya sheria ya
ulipaji wa ada.
Uwepo wa vyuo vinavyostahili kutoa elimu mahususi pamoja na
kutambulika kimataifa, hii ni kutokana na vyuo vilivyopo bado havitambuliki
kimataifa nafasi inayofanya kukosa nafasi za kazi nje ya mipaka, pamoja na hilo
tozo zinazotozwa kwa makampuni yanayopeleka watalii polini.
Hata hivyoUharibifu
wa mazingira unaotokana na tabia nchi,umeonekana nayo kuleta madhara katika
sekta ya utalii nchini hii inaweza kuepushwa enadpo nafasi ya utoaji elimu kwa
watu wanaoishi pembezoni mwa maeneo ya mbuga bado inanafasi kwa wananchi hao
ili waweze kuyatunza.
Vilevile Ujangiri, unaharibu sifa nzuri ya nchi yetu hali
hii inawafanya wanaopeleka watalii kwenda kuangalia wanyama kuona haibu kutokana na baadhi ya wanyama kutokuwepo
na kutoweka.
Naye
wadau wa sekta ya utalii wakiwemo wapagazi waliowakilishwa na katibu wao Leshee
Mollel ambaye ameeleza kuhusiana na kitengo chao kinavyokumbana na matatizo
mbalimbali ikiwemo kutopata haki zao za msingi ikiwemo mishahara.
Katibu
wa Wapagazi; mara kadhaa wamekuwa watu wanaobeba mizigo ya watalii kuelekea
sehemu mbalimbali za kitalii mfano kubeba mabegi yenye uzito unaokadiriwa mpaka
kufikia kilo 30 na kupanda nao mlima Kilimanjaro. Kazi ya kubeba mizigo ya
watalii ni nzito sana maana magari hayawezi kufika.
WAJIBU
WA VYOMBO VYA HABARI KATIKA SEKTA YA UTALII:
Mwenyekiti
wa jukwaa la wahiriri nchini Nevile meena, amezungumzia mambo kadhaa huku
akigusia majukumu ya uandishi wa habari katika kuwakilisha habari kwa umma,
kuanzia upatikanaji, mtu wa kwanza kutoa habari ni mwandishi mwenyewe, wakati chombo
cha habari kinasimama katika muhimli wa nne wa sheria katika nchi bado
mwandishi ana nafasi kubwa kuelemisha na kupeleka habari kwa jamii huku ndiye
mtu mwenye ukaribu wa mwananchi.
“Bahati mbaya
mwandishi wa habari wa nchini anapenda kuajiliwa kutokana na malipo tofauti na mwandishi aliye nchi za
ulaya ambaye yeye anapewa malipo makubwa kama ni mwandishi binafsi, vilevile mwandishi
anapaswa kuwa wa kwanza kufaham iwe mvua hama jua na kwa mazingira yoyote
kupata habari”Alisema Meena.








Post a Comment