0
Chanjo hizo ni zile ambazo huwa zinatolewa kwa watu wanasafiri nje ya nchi kama kinga kwa ajili ya homa manjano.

Profile Photo.

DAR ES SALAAM.
WATU saba, akiwamo mmoja anayedaiwa kuwa daktari bandia, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa madai ya kutengeneza kadi bandia za chanjo ya homa ya manjano na kuziuza kwa watu wanaofika hospitali ya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kupata huduma hiyo.

Kamishna wa Kanda hiyo, Simon Sirro, akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alimtaja aliyejifanya daktari kuwa ni mfanyabiashara Salum Natali (47), mkazi wa Chanika Magengeni, aliwataja watuhumiwa wengine ni walinzi watatu ambao ni Aisha Hassan (29) mkazi wa Vingunguti Mikoroshini, Yakobo Msenga (42) mkazi wa Chanika na Junith Dunstan (23) mkazi wa Kiwalani.

Wengine ni Oliver Bwegege (58) mkazi wa Kigogo Mkwajuni, mjasiriamali Fredy Nyomeye (44) mkazi wa Chang’ombe na fundi umeme Mohamed Bwanga (59) mkazi wa Majohe Gongo la Mboto.

Alisema watu hao walikamatwa Januari 16, mwaka huu majira ya saa 11:00 asubuhi baada ya mtoa taarifa (jina linahifadhiwa) kufika hospitalini hapo na kutakiwa kutoa fedha na mmoja wa watuhumiwa hao ili kupatiwa kadi hiyo ya chanjo ya homa ya manjano.

Katika mahojiano, watuhumiwa hao walikiri kufanya kosa hilo la kughushi na kutoa kadi hizo za chanjo pasi na mtu kuchomwa sindano yenyewe ya chanjo, alisema.

Kamishna Sirro alisema Natali alikuwa akijifanya kuwa ni daktari aliyekuwa akiwachoma watu sindano, aliongeza kuwa uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea ili kuwabaini washiriki wengine katika mtandao huo wa utoaji wa kadi hizo bandia za chanjo bila kutoa chanjo yenyewe husika.




Source NIPASHE.

Post a Comment

 
Top