0
Photo Profile: Mfano wa kisu ila hakihusiki.
Baadhi ya ndugu wa jamaa waliokatwa vichw wakiwa katika majonzi.
Wanachama na wahalifu wa magenge tofauti huzuiliwa katika magereza tofauti nchini Brazil
BRAZIL
Genge moja la uhalifu linaloendesha shughuli zake katika magereza mbalimbali nchini Brazil, limewakata vichwa takriban wafungwa 33 katika gereza moja kwenye jimbo lililopo Kaskazini la Roraima.
Ni tukio la pili chini ya juma moja kutokea nchini Brazil, ambapo maofisa wa Serikali wanaamini kuwa kukatwa vichwa huko kunatokana na mzozano unaondelea miongoni mwa wanachama wa genge hilo lijulikanalo kama PCC.
Gereza hilo lililosongamana liko eneo la mashambani, nje ya mji mkuu wa jimbo wa Boa Vista na hadi kufikia sasa maiti 31 zimepatikana na nyingi ya maiti hizo zimekatwa vichwa au kukatwakatwa vipande.

Maofisa wa Serikali wanasema ghasia hizo ni sehemu ya juhudi za magenge kuwa na mamlaka katika baadhi ya magereza.

Post a Comment

 
Top