0
Mindi Kasiga –Wizara ya mambo ya nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Kikanda na kimataifa kutoka kitengo cha mawasiliano.

DAR ES SALAAM.
Mpango wa taifa wa maendeleo wa mwaka 2016-2020 na ahadi za serikali ya rais Magufuri katika kipindi chake ni kuwa na uchumi wa viwanda, waziri wa mambo ya nje wa china Mh. Wang Yi anatarajiwa kuufanya ziara ya kikaziya siku moja hapa nchini mnamo Januari 09.2017 ambapo atapokelewa na mwenyeji wake waziri wa mamabo ya nje Balozi Dtr Augustine Maige.
.
Madhumuni ya ziara hiyo ikiwa ni kukuza mahusiano ya kihistoria kati ya nchi hizi mbili Tanzania na china uliodumu zaidi ya mika hamsini, hata hivyo mh. Wang Yi atafanya mazungumzo na mwenyeji wake Dtr Maiga kuhusu ushirikiano wan chi hizi mbili pia waziri huyo wa china atakutana na Rais Magufuri kwa lengo la kumsalimia.

Desemba 2015 itakumbukwa kuwa mkutano wa wakuu wa nchi za afrika na china china iliichagua Tanzania kuwa miongoni mwa nchi nne za afrika zitakazowezeshwa kupiga hatua kwenye maendeleo ya viwanda, mbali na mradi mkubwa wa ujenzi wa viwanda 200 unaoendana na mpango wa serikali wa viwanda vinavyotarajiwa kuwekezwa kwa kujengwa hapa nchini kabla ya 2020, China imeahidi kuisaidia Tanzania kuboresha Reli ya TAZARA, Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo pamoja na ujenzi wa Reli ya kati.


Masuala ya Amani na usalama katika eneo la Afrika masahariki yatazungumziwa kwa kina pamoja na mawaziri hao wawili watagusia nyanja ya kimataifa ikiwa ni pamoja na mageuzi ya Balaza la Usalama LA Umoja wa Mataifa, ambapo china inaunga mkono msimamo wa Afrika na wa Tanzania wa kutaka Afrika ipewe viti viwili vya kudumu katika balaza hilo.

Post a Comment

 
Top