0
Mwenyekiti anayemaliza muda wake Imani Matabula akiongea na wanashirikisho wa vyuo vikuu
hawapi pichani pamoja na kuwaaga kutokana na kumaliza muda wake.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa shirikisho la vyuo vikuu wakiwa tayari kufanya
uchaguzi kuwachagu viongozi wao wapya kwa kipindi kipya.
Mmoja wa wagombea wa nafasi ya uenyekiti Juvenile Jacka (Kulia) akiomba
kura kwa wajumbe wa mkutano mkuu washirikisho la vyuo vikuu mkoa wa
Dar Es Salaam mapema leo mchana katika ukumbi wa hotel ya Lamada.
Mwenyekiti wa Shirikisho la vyuo vikuu mkoa wa Dar Es Salaam Iman Matabula
(kulia) Mganwa Mzebwa –Katibu Hamasa shirikisho vyuo vikuu Taifa
na Debora Charles Katibu msaidizi wa shirikisho
Baadhi wa wajumbe wakisikiliza ahadi za mmoja wa wagombea (hayupo pichani)
mkutano mkuu wa shirikisho la vyuo vikuu wakiwa tayari kufanya
uchaguzi kuwachagua viongozi wao wapya kwa kipindi kingine.

DAR ES SALAAM
Mkutano mkuu wa wanachama wa ccm shirikisho  la vyuo vikuu nchini mkoa wa Dar es salaam unafanya uchaguzi  wa kuwachagua viongozi wa shirikisho leo jijini Dar es salaam  mara baada ya viongozi wanaomaliza muda wao wa uongozi wa mwaka mmoja kumalizika.

Akiongea   na wajumbe wa chama cha mapinduzi katika mkutano huo wa kuwachagua viongozi wapya mwenyekiti wa shirikisho anaemaliza muda wake Bw. Imani Matabula amesema kama kiongozi ni vema kuwa mstahimilivu katika kila jambo kwakuwa uongozi ni utumishi hivyo ni lazima kukubali kukosolewa ili kujenga nafasi ya uongozi bora.


Ameongeza kuwa ni vema kiongozi kuwa na nidhamu kwa wananchi, kuwaheshimu  na kuwajali kwa misingi ya katiba na kuwataka wajumbe wa shirikisho kuwapima wagombea wanaowania nafasi hizo kwa uwezo wao, hekima  na mikakati waliyonayo.

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

HABARI BAADA YA UCHAGUZI:
Katika uchaguzi huo uliofanyika jana kwa wagombea kuomba kura kutokana nafasi zao, ulichukua muda wa masaa mengi mpaka kukamilika kwake ambapo mpaka kufika saa 2200 usiku ndipo majina kura zilitangazwa na kupatikana kwa viongozi watakaoendeleza kurudumu la kiungozi kwa kipindi kijacho.

Jumla ya wagombea zaidi ya kumi na nafasi zilizokuwa zinahitajika ni tano, Mwenyekiti, Katibu, Katibu mwenezi, Katibu uchumi na fedha na Ktibu hamasa ambapo katika nafasi hizo walioshinda nagfasi hizo ni kama ifuatavyo;

1.     Fredrick Ludovic –Mwenyekiti Seneti Mkoa.
2.     Rahma Hassan –Katibu Seneti Mkoa.
3.     Kihaka Adam –Katibu Mwenezi Seneti Mkoa.
4.     Evance Kirumbi –Katibu Uchumi na Fedha.

5.     Yassin O. Makaraba –Katibu Hamasa.



Post a Comment

 
Top