0
Afya ya jamii imekuwa ikipiganiwa kwa kiasi kikubwa kwa nchi na mataifa kutokana na kuwa na umuhimu wa pekee kwa wananchi wa sekta zote, kwa mfano kujadili swala la hedhi hadharani limekuwa ni kinyume na utamaduni wa watu wa taifa lolote hasa la kiafrika.

Ndekela Mazimba anasema kuwa siku hiyo inamsadia kukabiliana na uchungu wa hedhi.
Mutinta Musokotwane –Chikopela yeye anasema kuwa tayari Zambia kuna siku nyingi zana za rikizo hata siku ya maombi.
Justin Mukosa (kushoto) yeye anaunga mkono sheria hiyo akiwa na bi Mazimba -kulia.




ZAMBIA.
Nchini Zambia hii inaweza kuonekana ni kwenda kinyume na maadili ndio maana kuna sheria za wafanyakazi zinazowaruhusu wanawake walio katika hedhi kuchukua siku moja ya mapumziko inayojulikana 'Mother’s day' licha ya kwamba inasimamia wanawake wote iwapo wana watoto au la.
Sheria hiyo haina masharti, wanawake wanaweza kuchukua siku hiyo kwa matakwa yao wenyewe na sio lazima watoe kithibitisho chochote cha kimatibabu, hatua inayowalazimu wengine kuhoji kuhusu sheria hiyo.
Ndekela Mazimba ambaye anafanya kazi katika idara ya mahusiano ya umma anasema, ''Nadhani ni sheria nzuri kwa sababu wanawake hupitia mengi wakati wanapokuwa katika hedhi''. Bi Mazimba hajaolewa wala hana watoto lakini huchukua siku yake ya Mother’s Day kila mwezi kutokana na uchungu anaopata wakati anapoingia katika hedhi.
''Unaweza kubaini kwamba katika siku yako ya kwanza ya hedhi, unaweza kusikia maumivu mengi katika tumbo, unaweza kununua dawa zote za kutuliza maumivu lakini unasalia kitandani siku nzima, na mara nyengine, unagundua kwamba watu wengine wanahisi uchungu siku za kwanza za hedhi, lakini siku zinaposonga uchungu unapungua.Mimi hutaka kusaidiwa kwa siku za kwanza wakati ninahisi uchungu mwingi'',alisema Mazimba
Wanawake nchini Zambia hawalazimiki kufanya maandalizi yoyote kabla ya kupumzika siku hiyo, lakini wanaweza kupiga simu siku hiyo kusema wanachukua Mother’s day, lakini muajiri anayemnyima mfanyakazi wake siku hiyo anaweza kushtakiwa.
Justin Mukosa ambaye amemuajili bi. Mazimba anaunga mkono sheria hiyo na kusema kuwa anaelewa matatizo ya wanawake wanayokumbana nayo wanapopima kati ya majukumu ya kifamilia na kazi, anasema hatua hiyo inaweza kuwa na athari nzuri kwa kazi za wanawake.
''Utendaji sio tu mtu aliye afisini. Unafaa kupimwa kulingana na uzalishaji wa mtu huyo''.
Lakini anakiri kwamba kuna matatizo katika mfumo huo kutokana na kuwakosa wafanyakazi kupitia notisi fupi mbali na majaribio ya watu kuuchezea. Unaweza kutumiwa vibaya kwamba pengine mtu ana jambo lake ambalo anataka kufanya kwa hivyo anachukua Mother’s day.
Sio kila mtu anaunga mkono siku hiyo ya Mother’s Day na kuna wanawake wengi miongoni mwao wanakosoa, Mutinta Musokotwane-Chikopela ameolewa na ana watoto watatu, anafanya kazi ya ukuzaji lakini hachukui siku ya mother’s day akisema kuwa inasababisha uvivu miongoni mwa wafanyikazi wanawake.''Siiamini na siichukui, hedhi ni jambo la kawaida katika mwili wa mwanamke, ni sawa na kuwa na mimba ama hata kujifungua'',alisema.
Nadhani wanawake huchukua fursa ya siku hiyo hususani kwamba hakuna njia ya kuthibitisha kwamba uko katika hedhi au la.
Bi Chikopela anasema kuwa sheria hiyo inafaa kufanywa kuwa wazi zaidi, ''Tatizo la Zambia ni kwamba kuna likizo nyingi sana, ikiwemo likizo ya siku ya maombi, kwa hivyo nadhani Mother’s day inawafanya wale wanaopenda likizo kufurahi''.



Source: BBC

Post a Comment

 
Top