![]() |
| Gavana Kivutha Kibwana wa Makueni. |
NAIROBI.
Kwa muda sasa wabunge na maseneta
wamesikika wakitoa matamshi ya kukejeli maagizo ya mahakama na ushauri wa
mwanasheria mkuu wa serikali, visa vya hivi karibuni ni tukio la kuwahoji mawaziri
mbele ya kikao cha bunge, vilevile maagizo ya mahakama kuhusu kutimuliwa kwa
Gavana Kivutha Kibwana wa Makueni nchini Kenya.
Maseneta hao wamekuwa wakilalamikia kutishiwa na polisi waliokuwa wamelizingira
jengo ya bunge la seneti la nchi hiyo, lakini wajuzi wa sheria wanasema mienendo
hiyo inafaa kukoma kwa kuwa ni mfano usiofaa kwa wakenya, aidha,
polisi waliweka vizuizi mbalimbali katika barabara ya kuingia bungeni.
![]() |
| Profile photo: Ukumbi wa bunge la kenya. |
Maseneta hao walikuwa
wamekusanyika kwa ajili ya kikao maalum cha kujadili sheria ya uchaguzi,
wameeleza kughadhibishwa na hatua ya polisi kuwadhalilisha bungeni, vile vile wamejitetea
kuwa polisi waliojihami walimiminika sehemu mbalimbali ya bunge hilo, jambo si la
kawaida.
"Tunalaani vikali hatua ya polisi kuzingira bunge la Seneti
na yeyote aliyehusika kuwapa mamlaka ya kuzingira bunge siku hii, anastahili
kuchukuliwa hatua". Alisema
kiongozi wa waliowengi katika Seneti, Kithure Kindiki.
Seneta kutoka mrengo wa
serikali, Kipchumba Murkomen, alisifu hatua ya kuwepo kwa polisi hao na akasema.
"Tujilaumu
wenyewe kwa mienendo yetu, tunaingia bunge tukibeba visu, pilipili na hata filimbi
wabunge wenzetu wanamtusi Rais ni aibu".
Siku kadhaa zilizopita, bunge la taifa hilo lilishuhudia vurugu baada ya wabunge wa upinzani kujaribu kumzuia spika Justin Muturi kuingia bungeni wakipinga mjadala wa kubadilisha sheria za uchaguzi. Hata hivyo seneta Hassan Omari alipendekeza kikao hicho kivunjwe hadi polisi watoke bungeni.
Siku kadhaa zilizopita, bunge la taifa hilo lilishuhudia vurugu baada ya wabunge wa upinzani kujaribu kumzuia spika Justin Muturi kuingia bungeni wakipinga mjadala wa kubadilisha sheria za uchaguzi. Hata hivyo seneta Hassan Omari alipendekeza kikao hicho kivunjwe hadi polisi watoke bungeni.


Post a Comment