![]() |
Profile Photo: Mbunge Lema mwenye gwanda jeusi akiongozwa na askari wa jeshi la magereza huku wananchi wakishuhudia. |
![]() |
Profile Photo: Godbless Lema akipanda kwenye Landrover ya Polisi kutokea kituo cha polisi mjini Arusha. |
ARUSHA.
Mbunge Arusha mjini kwa tiketi ya chama cha demokrasia
na maendeleo -Chadema Godbless Lema akiwa anaendelea kukaa na kupata madhira
kwa kukaa lupango, huku ikionekana hata mwaka mpya ataushuhudia akiwa huko
mawakili wake wamelalamika kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kuwasilisha hoja
yao mahakama kuu kanda ya Arusha.
Peter
Kibatala amabaye ni mmoja kati ya mawakili wanaomtetea mbunge huyo amesema kuwa
upande wa serikali badala yake umepeleka notisi mahakama kuu ya kukata rufaa
ili kuendelea kuchelewesha utaratibu wa Lema kupewa dhamana. "Tayari upande wa mashtaka wameshaona kwamba
Mahakama kuu inaelekea kusikiliza hoja ya ziada ambayo upande wetu ni kuwa
mteja wetu kunyimwa dhamana na mahakama ya chini," alisema kibatala.
Wakili Kibatala ameendelea kusema kuwa kama
inavyojulikana mahakama ya rufani huwa haikutani kwa haraka na wakati mwingine
inachukua miezi minne, sita hama mwaka mzima, kitu ambacho kitamuacha mteja wetu
akae jela kwa muda huo wote na kuwa kesi ambayo awali ilipangwa Januari 2 hivi
sasa haitakuwepo na hivyo wanasubiri uamuzi wa mahakama kuu utakaotolewa
Januari 4 mwaka ujao 2017.
Mbunge
huyo anashtakiwa kwa kutumia lugha ya kuchochea inayoweza kusababisha hali ya
sintofahamu inakumbukwa mnano Novemba 11, hakimu mkazi alimpa Lema dhamana
lakini kabla ya kutoa masharti ya dhamana hiyo, upande wa serikali ulitoa
notisi ya kukata rufaa, hata hivyo Kibatala alisema upande wa utetezi tayari
wameshawasilisha hoja zao Ijumaa kama walivyotakiwa na mahakama kuu.
Katika hati ya maandishi yenye kuelezea hoja za
upande wa Lema inaeleza kuwa wamesikitishwa na kitendo cha serikali
kutowasilisha hoja yao kuhusu ombi la kunyimwa dhamana kwa mteja wao waraka huo
umeendelea kueleza kuwa kitendo cha upande wa serikali kutowasilisha hoja yao
ya maandishi ni sawa na kutofika mahakamani, na hivyo ni wazi kwamba linapelekea
rufaa kutupiliwa mbali.
Mawakili wa mbunge huyo Jumatano iliyopita
walikubali rufaa ya serikali kuanza kusikilizwa kwa njia ya maandishi, "Tumeona
kuwa matokeo ya rufaa ni moja, rufaa ya Lema isimamishwe mpaka pale rufaa ya
serikali itakapowasilishwa katika mahakama kuu," alisema Bw. Kibatala.
Jaji wa mahakama kuu alitoa nafasi kwa pande zote
mbili kuwasilisha hoja za ziada, na kuwa wao wataendelea kusimama pale pale
kwamba wanapinga uamuzi wa mahakama hiyo ya chini kumnyima mteja wao dhamana.
Source: VOA
Post a Comment