0

Profile photo: Mwanga unawake kwenye giza na kuleta nuru.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Felix Ngamlagosi akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mapema leo, kushoto ni kaimu mkurugenzi wa umeme, Godfrey Chibulunje na meneja mawasialiano wa mamlaka, hiyo Titus Kaguo.




DAR ES SALAAM.
Kupanda kwa garama ya maisha kuna njia nyingi zinazosababisha ikiwemo vyakula, usafiri na mahitaji mengine ya msingi na yasiyo ya msingi.

Kwa mazingira ya kawaida ubo mahitaji muhimu kama umeme kwa maendeleo ya taifa lolote lazima kuwepo nauboleshaji wa baadhi ya vitu muhimu, shirika la umeme nchini Tanesco liliomba kupandisha garama za umeme toka mwezi wa Oktoba 4.2016, kwa asilimia 18.19% kuanzia tarehe 01.01.2017.


Ambapo katika pendekezo hilo linalenga kuongeza bei ya sasa ya umeme kutoka shs 242.2 kwa unit mpaka shs 286.28 kwa unit, ambapo pendekezo hili linaonyesha mgawanyiko kwa uzalishaji wa umeme shs 155.35unit kusafirisha shs 23.76unit na kusambaza shs 107.17unit, hata hivyo pamoja na kuwepo kwa ushauri kutoka mabaraza ya watumiaji kutoa ushauri kwa Tanesco kuacha kupandisha garama, ushauri huo umefanyiwa kazi katika hatua kadhaa.

Baadhi ya watumiaji wa nishati hiyo kupitia balaza la ushauri la seriakali -GCC, balaza la watumiaji wa huduma zinazodhibitiwa na EWURA –EWURA CCC, Shirika la umeme la Zanzibar –ZECO, Mamlaka ya maji singida, Kiwanda cha saruji cha Simba na wananchi kwa ujumla, walitoa mapendekezo yao kupinga kuongeza garama hizo kutokana na muda mfupi tu umepita ambapo waliomba kupunguza garama za umeme.

 Pamoja na uchambuzi wa kina EWURA imejiridhisha kuwa bei inayopendekezwa na TANESCO kwa mwaka 2017 ni ya juu kama inavyoelezwa lakini kutokana na kutambua garama za haki tuzinazoingiwa na TANESCO ndiyo zinazingatiwa, hivyo gharama za uendeshaji zilipunguzwa kutoka zile zilizoombwa na TANESCO shs 286.23 na kurudi kufikia shs 263.02 kwa unit.

Vilevile mgawanyo mpya wa watumiaji wa watumiaji wa nishati hiyo utakuwa katika makundi tofauti, kuna D1 hawa ni watumiji wadogo wanaotumia umeme chini ya 75unit, T1a wateja wa kawaida ambao ni wa majumbani, biashara na taa za barabarani lakini pia kuna T1b –Viwanda vidogo nk, kutokana na mgawanyo huo garama zitaongezeka kulingana na mtumiaji kwa kundi alilopo.

Post a Comment

 
Top