 |
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akiongea
wakati wa hafla ya kutiliana sahihi za kuanza kwa mradi wa uboreshwaji wa
barabara na miundombini jijini Dar Es Salaam.
|
 |
Mwakilishi wa kampuni ya China Railway 7th
Construction wa kulia akibadilisha dodoso za mradi na Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema kushoto mara baada ya kuweka sahihi za kuanza kwa mradi.
|
 |
Baadhi ya wawakilishi kutoka serikalini, mstahiki meya Chales Kuyeko mwenye miwani , Mkuu wa wilaya
Sophia mjema mwenye gauni jekundu, mwakilishi wa kampuni iliyopewa kazi ya
ujenzi wa miundombinu ya CR7C aliyenyanyua dodoso wakiwa katika picha ya
pamioja mara baada ya kutiliana saini mkataba.
|
DAR ES
SALAAM.
Mradi mkubwa wa uboleshaji wa miundominu
katika manispaa ya wilaya ya Ilala utakaofanyika kwa awamu kadhaa na
unaofadhiliwa na Benki ya Dunia unatarajiwa kuanza kutekelezwa mara baada ya
kusainiwa kwa utekelezaji wake leo katika ukumbi wa Anatouglo mnazi mmoja
jijini Dar Es Salaam.
Mradi huo unaotarajiwa kutekelezwa kwa mwaka mmoja unahusu barabara zisizo za lami na
utaanza kwa hatua ya uboreshajina ujenzi wa miundombinu ya madaraja na
barabara za mitaani zinazounganisha mitaa kama ile ya Olimpio yenye urefu wa
0.2km iliyopo upanga, baadaye kurekebisha na kuweka mitaro na baadaye
kurekebisha mitaa kupitia hatua kadhaa zilizopo tayari.
Wakati wa kusaini mkataba huo, mkuu wa
wilaya ya Ilala Sophia Mjema amemuagiza mkurugenzi wa manispaa ya ilala
Msongela Nitu na mstahiki meya Charles Kuyeko kusimamia kikamilifua mradi huo
uwe wa viwango vya hali ya juu na
usije kuwa wa kurudiarudia.
Utiaji sahihi umefanyika kati ya halmashauri
hiyo na kampuni iliyopewa ukandarasi ya China Railway Seventh Group mbele
ya viongozi kadhaa wa serikali na wawakilishi wa benki dunia pamoja na mstahiki
meya na viongozi wengine.
DC
Mjema amefafanua kuwa mradi huo wa DMDP utapendezesha mitaa na kuondoa foleni
jambo ambalo litawasaidia wananchi wa maeneo husika kupunguza muda wa kwenda
katika shuguli zao, hivyo amewahimiza mkurugenzi na mstahiki Meya wa ilala
kuhakikisha kuwa barabara na madaraja yanajengwa kwa viwango na kwa wakati kama
ilivyopangwa.
DC Mjema ameeleza kuwa
mradi huo utazipitia barabara za Ndanda, Olympio, Kiungani, Omary Londo na
Mbarouk ambazo zote zitakuwa na urefu wa kilomita 2.8 kwa kila moja, ambapo
katika hatua nyingine DC Mjema amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuhakikisha
maroli yaliyozidi kiwango cha kubeba mizigo hayapiti kwenye miundombinu hiyo
kwani yataleta uharibifu.
Kwa upande wake
Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Charles Kuyeko ameeleza kuwa watajitahidi
kuusimamia kikamilifu mradi huo wa DMDP ambapo zaidi ya bilioni 11.1 zimetengwa
na Benki ya Dunia kwa ajili ya Mradi huo, huku Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo
Msongela Nitu akihaidi kuyafanyia kazi maagizo yote ya Mkuu wa Wilaya.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.