![]() |
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akiongea
wakati wa hafla ya kutiliana sahihi za kuanza kwa mradi wa uboreshwaji wa
barabara na miundombini jijini Dar Es Salaam.
|
![]() |
Mwakilishi wa kampuni ya China Railway 7th
Construction wa kulia akibadilisha dodoso za mradi na Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema kushoto mara baada ya kuweka sahihi za kuanza kwa mradi.
|
DAR ES SALAAM.
Mradi mkubwa wa uboleshaji wa miundominu
katika manispaa ya wilaya ya Ilala utakaofanyika kwa awamu kadhaa na
unaofadhiliwa na Benki ya Dunia unatarajiwa kuanza kutekelezwa mara baada ya
kusainiwa kwa utekelezaji wake leo katika ukumbi wa Anatouglo mnazi mmoja
jijini Dar Es Salaam.
Mradi huo unaotarajiwa kutekelezwa kwa mwaka mmoja unahusu barabara zisizo za lami na
utaanza kwa hatua ya uboreshajina ujenzi wa miundombinu ya madaraja na
barabara za mitaani zinazounganisha mitaa kama ile ya Olimpio yenye urefu wa
0.2km iliyopo upanga, baadaye kurekebisha na kuweka mitaro na baadaye
kurekebisha mitaa kupitia hatua kadhaa zilizopo tayari.
Wakati wa kusaini mkataba huo, mkuu wa
wilaya ya Ilala Sophia Mjema amemuagiza mkurugenzi wa manispaa ya ilala
Msongela Nitu na mstahiki meya Charles Kuyeko kusimamia kikamilifua mradi huo
uwe wa viwango vya hali ya juu na
usije kuwa wa kurudiarudia.
Utiaji sahihi umefanyika kati ya halmashauri
hiyo na kampuni iliyopewa ukandarasi ya China Railway Seventh Group mbele
ya viongozi kadhaa wa serikali na wawakilishi wa benki dunia pamoja na mstahiki
meya na viongozi wengine.
Post a Comment