![]() |
Naibu waziri Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano mh. Edwin Ngonyani |
Naibu waziri Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano mh. Edwin Ngonyani amewaasa watendaji wa wizara hiyo
kuzingatia nidhamu ili kuleta tija na ufanisi katika maeneo yao ya kazi pamoja
na kuwahusia kuwa ikiwa mtumishi atakosa nidhamu ni wazi anazorotesha ufanisi
sehemu ya kazi, maana nidhamu ni kiungo muhumu katika kupata mafanikio.
“uwepo wa migogoro baina ya watumishi
sio tu ni ukosefu wa nidhamu bali pia ni kikwazo kikubwa katika kuleta ufanisi
mahali pa kazi…” amesema Naibu Waziri,
Edwin Ngonyani.
Hata hivyo ametoa rai
kwa vingozi kufanya kazi kwa uwazi kwa kuthamini michango ya wanao waongoza na
amesisitiza kuwa haipendezi kuona mambo yanayoendelea sehemu ya kazi ilihali
watumishi wenyewe hawajui kinachoendelea “tuache tabia za ubwana bali tuongoze walio chini yetu
kistaarabu kwa uadilifu mkubwa na kwa ridhaa yao, tukifanya hivyo tutapunguza
kama sio kuondoa manung’uniko na migogoro katika sehemu zetu za kazi” Alisema.
Kwa upande mwingine
ametoa amegusia mjadala utakaohusu mambo kadhaa kama; kupitia na kupitisha
miundo ya watumishi na mgawanyo wa kazi, taarifa za saccos –taa na uzinduzi wa
katiba ya chama cha kufarijiana pamoja na taarifa za utendaji ambapo kupitia mijadala hiyo italeta suluhisho la
changamoto zinazowakabili katika kufikia malengo yao.
Post a Comment