0
Watu wakiwa wamerejea katika kazini ili kuendelea kuwajibika kutoka katika mapumziko ya krismasi, huku wakijipanga kukaribisha mwaka mpya, baadhi ya raia katika nchi za ughaibuni, sikukuu hiyo imewaacha katika majonzi makubwa baada ya kupatwa na dhoruba ya kuondokewa na ndugu zao.




.Moja ya eneo ambalo lilikumbwa na shambulizi katika mji wa Chicago nchini marekani
likiwa chini ya uangalizi wa polisi

Maofisa usalama wakiondoa mwili wa raia aliyejeruhia katika eneo la shambulizi.


HABARI KWA UNDANI:
MAREKANI.

Watu wapatao 11wameuwawa na wengine 37 wamejeruhiwa wakati wa maadhimisho ya Krismasi mwishoni mwa wiki iliyoisha, asubuhi mapema siku ya krismasi pekee watu watano waliuawa na mwingine 11 walijeruhiwa, taarifa ya polisi katika mji wa chikago lilipotokea shambulio hilo walisema.

Idadi hiyo ya watu waliouawa imefanya jumla ya watu waliouawa kwa risasi katika kipindi cha mwaka 2016 kufikia 750, na kufanya mji huo wa chicago kuongoza kwa mauaji katika kipindi cha miongo miwili.
Matukio kama haya yamekuwa yakitukio sehemu kadhaa na wauaji wakitokomea kusikojulikana, Polisi nchini humo wamesema pia kwamba watu zaidi ya 30 wamejeruhiwa katika mashambulizi hayo yaliyohusisha bunduki, na kuyahusisha na magenge ya uhalifu.
Kutokana na tukio hilo hakuna mtu alikuyekamatwa kwa shambulizi hilo. Pia mwishoni mwa wiki, watu watatu waliuawa na wengine tisa walijeruhiwa kati ya Jumamosi na mapema Jumapili, na watu wengine watatu waliuawa na 17 walijeruhiwa siku ya Ijumaa na asubuhi ya Jumamosi ya sikukuu.



Post a Comment

 
Top