0
Moja ya mti wa krismasi ambao mara kadhaa baadhi ya wakristo wamekuwa wakiutumia kwa kupamba katika nyumba zao.




Wakazi wa jijini la Dar Es Salaam wakifurahia sikukuu ya krisimasi katika ufukwe wa bahari ya hindi eneo la Ununio Beach


Mchungaji Kombo akimbatiza mtoto Comfort Innocent
Moshi wakati wa ibada ya krismasi katika kanisa la 
Kiinjili  la kilutheli usharika wa Boko jijini Dar eS Salaam.
DAR ES SALAAM.
Tukio la kuzaliwa Yesu Kristo miaka zaidi ya 2000 iliyopita, limekuwa likisherehekewa na kuadhimishwa na baadhi ya wakristo duniani kote (tunasema baadhi ya wakristo ikiwa na maana kuna baadhi wasioamini kuzaliwa kwa kristo disemba 25.12.) Na sehemu ya wakristo wasiomani tarehe hizo ni waadventisra wasabato.

Hivyo basi nchini Tanzania tukiwa ni sehemu ya dunia watanzania wamesherehekea siku hiyo pamoja na kuwepo changamoto mbalimbali baadhi wakidai zinatokana na ukata wa fedha ikiwa ni tofauti na miaka iliyopita, hali hii inasemwa inatokana na mazingira yanayochagizwa na hali ya uchumi wa mtu mmoja mmoja kwa kipindi hiki.
                                                                              
TODAYS NEWS ilipata nafasi ya kuhudhulia moja ya ibada katika kanisa la kiinjili la kilutheli ushirika wa Boko jijini Dar Es Salaam ambapo katika misa ya krismasi iliyoendeshwa na mchungaji Boniface kombo ambaye ni naibu katibu mkuu wa dayosisi ya mashariki na pwani ametoa wito wa kuwa na Amani kutokana na Yesu alipozaliwa alikuja kuunganisha na si kubomoa, hivyo basi kila mtu ana wajibu wa kutambua ikiwemo kusherekea huku akiwa na wajibu wa kutunza amani.


Katika kuonyesha umuhimu wa Amani nchini, afrika na duniani, sauti ilisikika ndani ya kanisa hilo la KKKT DMP –Boko kutoka kwa kwaya kuu ya kanisa hilo ilipokuwa ikiimba wimbo unaoitwa ‘MAANA KWA AJILI YETU’ ambao moja ya beti zake zilisikika zikisema; **Tanzania yahitaji sana mtawala wa Amani na magombano yasiwepo, katika nchi yetu tumwombe sana Mungu ufalme wake ushuke (ili tuishi kwa Amani siku zote) maishani mwetu’ aliyezaliwa mfalme wa Amani, Amani twahitaji, Tanzania Afrika na dunia nzima iokolewe.



Post a Comment

 
Top