DAR ES SALAAM
Watoto wasio na utapiamlo wanafaulu zaidi
kusoma masomo ya Kiswahili na Hisabati kuliko wale wenye utapiamlo.
Takwimu zilizokusanywa zinaonesha kuwa,
kwa ujumla kitaifa, asilimia 4 ya watoto wenye umri chini ya miaka 5, asilimia
5.6 ya watoto wenye miaka kati ya 5 na 9 na asilimia 5.7 ya watoto wenye miaka
kati ya 10 hadi 14 wana utapiamlo.
Hatahivyo kuna utofauti mkubwa kiwilaya:
asilimia 23.9 ya watoto wa Songea Mjini walio chini ya miaka 5 wana utapiamlo
ukilinganisha na asilimia 0.3 wilaya ya Tabora Mjini na Musoma Mjini.
Kitaifa, ni shule moja tu kati ya tano
inayotoa huduma ya chakula cha mchana shuleni (asilimia 23). Kwa mkoa wa
Kilimanjaro, asilimia 79 ya shule zinatoa chakula cha mchana lakini katika mkoa
wa Geita, ni asilimia 5 tu ya shule zinazomudu chakula cha mchana kwa watoto.
Post a Comment