![]() |
| Rais Dr. John Pombe Magufuri. |
DAR ES SALAAM.
Wafanyabiashara wa viumbe hai wa polini wamemuomba
Rais John Mugufuli asikie kilio chao na kufungulia biashara yao ya kusafirisha
viumbe hao nje ya nchi baada ya serikali kupiga marufuku usafirishaji huo tangu
mwanzoni mwa mwaka huu
Wafanyabiashara
hao walivamia Wizara ya Maliasili na Utalii na kuonana na Waziri mwenye dhamana
Prof.Jumanne Maghembe kuhusu kilio chao hicho cha kutaka serikali ifungulie
biashara hiyo ya uuzaji wa viumbe pori hai nje ya nchi.
Akizungumza kuhusu sakata hilo, Prof. Maghembe amesema kimsingi Serikali imepiga marufuku biashara ya
kusafirisha kuanzia Machi 17 mwaka huu, Serikali ilisimamisha ghafla usafirishaji wa
viumbe pori hai nje ya nchi, hatua iliyokuja baada ya wafanyabiashara hao
kulipia gharama zote wizarani ikiwemo vibali, hivyo wametaka rais kuingilia
kati jambo hilo.
![]() |
| Mjusikafiri anakimbia kwa wepesi wa aina yake. |
“serikali
imekataza kwa angalau miaka mitatu biashara hii iachwe ili idara ya wanyamapori
ijipange namna ya kufanya biashara hii kwa usalama, uhakika na kwa kufuata
sheria na sababu kubwa za serikali kuchukua hatua hiyo ni kwanza wanyama wa
Tanzania wanakamatwa katika bandari na viwanja vya ndege vya nje ya nchi wakiwa
hawakufuata taratibu za kusafirishwa.”amesema waziri Prof. Maghembe.
Pamoja na hayo Mh. Maghembe
amesema wataalamu wa wizara wanaendelea na uhakiki wa vibali vya
wafanyabiashara hao ili wajue namna ya kuwalipa kifuta jasho.


Post a Comment