0
Bunge la seneti nchini kenya limepitisha sheria kwa kampuni mashirika mbalimbali nchini humo kuweka sehemu maalum kwa ajili ya kuwanyonyeshea watoto wachanga.

Mbunge machachari mama Wangali ambaye ndiye chanzo cha kuwekwa sheria hiyo baada ya kusimama kidete kuanzishwa kwa sheria hiyo, alikuwa akikumbwa na hadha wkt akitaka kumpa chakula mwanaye mdogo.

Ameongeza kuwa imefika wakati jamii ielewe kuwa kunyonyesha mtoto mchanga si suala la kuona aibu hasa unapokuwa eneo lolote ilimradi mtoto akiwa na uhitaji wa kunyonyeshwa, bali iwe ni jambo la kawaida na kutoa mfano kwa mtu yeyote anayetaka kula, "inakuwaje pindi unapotaka kula na unafunikwa kichwa?"


Suala la unyonyeshaji limekuwa ni tatizo kwa miongo kadhaa sasa hususani kwa kizazi cha sasa kutokana na mazingira yalivyo, vilevile ikiarifiwa kwa kina mama kutakiwa kunyoshesha watoto kwa takribani miezi sita ya mwanzo mara baada ya kuzaliwa.

pamoja na kupitishwa kwa sheria hiyo bado kuna hoja kwa nini bunge hilo halijaweza kuwa mfano wa kuigwa kwa kuanza kuweka sehemu hiyo?

Post a Comment

 
Top