Mahakama ya Juu nchini Kenya imefutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika mapema mwezi uliopita katika uamuzi kuhusu kesi iliwasilishwa na muungano wa upinzani National Super Alliance.
Wakati uchaguzi huo umefutwa na kutarajiwa kufanyika baada ya siku 60, nchi ya Kenya kwa sasa inaingia katika historia ya pekee ikiwa ni pamoja na mahakama ya nchi hiyo kutoa maamuzi kwa kufuata sheria. YANAYOJIRI NCHINI HUMO KWA SASA.
Mgombea urais wa upinzani Raila Odinga amesema leo ni siku ya kihistoria kwa Kenya na kwa Afrika, kwa mara ya kwanza, Mahakama imefutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais.
"Tulisema tangu awali kwamba safari yetu ya Canaan haiwezi kuzuiwa. Siku ya tarehe 8 Agosti tulivuka mto Jordan."
Bw Odinga amesema upinzani hauna imani kwamba tume ya sasa ilivyo inaweza kuandaa uchaguzi huru na wa haki.
MUSYOKA: Heshima ya mahakama imerejeshwa
Makamu wa Rais wa zamani Kalonzo Musyoka amesema mahakama imekuwa mfano mwema kwa Afrika na dunia nzima.
"Ninajivunia kuwa Mkenya leo," amesema.
"Sasa tutaangalia kwa kina kuhusu tume ya uchaguzi. hatuna imani kwamba wanaweza kuandaa uchaguzi huru na wa haki."
PICHA CHINI: wafuasi walio upande wa Raila Odinga mjini Kisumu wakishangilia kufutwa kwa matokeo ya Urais.
Kusherehekea ushindi wa Odinga Nairobi
PICHA CHINI: Wafuasi wa kiongozi wa upinzani Raila Odinga jijini Nairobi wamekuwa barabarani wakisherehekea hatua ya mahakama kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa urais.
PICHA CHINI: Nje ya mahakama ulinzi mkali umewekwa na umendelea kuwepo hata sasa jijini Nairobi.
📍Zanzibar.Makamu wa pili wa Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Mh. Hemed Seleiman amefungua Kongamano la tano (5) la watoa huduma ya daw...Read more »
📍 Zanzibar.Kongamano la kimataifa la usimamizi wa biashara na maendeleo ya uchumi, limefunguliwa mjini Zanzibar na makamu wa pili wa Rais Mh. He...Read more »
📍 ARUSHA.Taasisi ya Sayansi ya Teknolojia Afrika ya Nelson Mandela imempokea mkuu mpya wa Taasisi hiyo baada ya aliyekuwa mkuu wa Taasisi hiyo Mh. Mo...Read more »
Zanzibar.
Waziri wa Maji Nishati na Madini Zanzibar Mhe. Shaib Hassan Kaduara amefunga Kongamano la Maji lililofanyika mjini Zanzibar kwa siku mbili, ...Read more »
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.