0
PHOTO: Aliyesimama: Godfrey Edward Afisa biashara
Arusha, kulia kwake  kwake ni Mwenyekiti wa Wanjamuco Alex Lasiki
.
ARUSHA.
Chama cha wauza nyama mkoa wa Arusha (WANJAMUCO) kimefanya sherehe ya kutimiza mwaka mmoja, akizungumza katika sherehe sherehe hiyo Afisa biashara wa mkoa Godfrey Edward aliyekuwa mgeni rasmi akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Arusha amesema, wakati ushindani wa biashara ya ng’ombe unazidi kuwa mkubwa na ng’ombe wengine wakisafirishwa nje ya nchi, serikali imekuwa inakosa mapato kutokana na kuwepo kwa madalali.

PHOTO: Baadhi ya wanachama wa wanaounda umoja wa wauza nyama jijini Arusha (WANJAMUCO) wakimsiliza Afisa biashara wa mkoa Geofrey alipokuwa akitoa hotuba. 

PHOTO: Picha ya pamoja wanachama wakiwa na viongozi wao mara baada ya sherehe nya kutimiza mwaka mmoja


HABARI KWA UNDANI.
Ameongeza kuwa Wanjamuco hao kuboresha umoja wao na kuweza kuthibiti biashara holela ya bucha za nyama ambazo zinazagaa mtaani na sehemu ambazo zisizofaa kuwekwa maduka ya nyama, “tukiwa na nia moja kwa kuweka mbele utoaji wa huduma bora na ushirikiano tutaweza kuthibiti mabucha yaliyo chini ya viwango” alisema Godfrey.

Wakati nchi ikiwa inaelekea katika uchimi wa viwanda, wauzaji hao wa nyama wameitaka serikali kuzuia uuzwaji wa mifugo nje ya nchi ili kuweka nafasi ya mazao gafi zitokanazo na mifugo kama ngozi, maziwa, pembe,kwato vizalishwe hapa nchini na kutumwa nje ya nchi kama bidhaa nyingine ili kukuza mapato na ajira nchini.

Naye mwenyekiti wa umoja huo Alex Lasiki amesema pamoja na changamoto nyingi zinazowakumba wauzaji wa nyama bado wanaiomba serikali kuweka mikakati itakayoweza kupata kodi kutoka kwa madalali wa mifugo wanaopata mapato kutokana na mifugo isiyo kuwa yao na ndiyo wanaosababisha kupanda kwa bei ya mifugo.

“tunaiomba serikali ituunge mkono kupiga vita biashara holela ya wauza nyama wanaokuja kwa msimu wanaosababisha tasnia ya nyama hasa tunazopeleka nje inaonekana haina kiwango, kwani nyama ni bidhaa ambayo ukiitumia vibaya inaweza kukudhuru” alisema Lasiki.

Pia wameiomba mamlaka ya mapato nchini TRA kutoa elimu juu yam ashine za kukusanyia kodi Efds ili kuweza kuepusha migangano inayoweza kujitokeza kutokana na ununuzi, uuzaji na upatikanaji wa mapato kwa wauzaji wa nyama mkoani Arusha.
Umoja huo wenye jumla ya wanachama 112 unawaunganisha wauzaji wa nyama mkoani Arusha ambapo kati ya hao 100 ndiyo walio hai katika kuchangia na kuhudhulia katika mikutano na shuguli mbalimbali za umoja huo.


Hata hivyo serikali imekuwa mstali wa mbele katika kuboresha na kuandaa mazingira mazuri ya usafirishwaji wa mifugo pamoja na mazao yatokanayo na mifugo ili kusafirshwa nje ya nchi ili kuweza kulinda mapato ya wafugaji, wanunuzi na wauzaji wa ndani.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top