0
DAR ES SALAAM.
Abilia waliokuwa wakisafiri kutoka mabibo kuelekea Makumbusho jijini Dar Es Salaam kwa kutumia usafiri wa daladala walijikuta wakikataa kubebeana mabegi mara baada ya kusikia taarifa za kuwepo kwa nyoka aliyeonekana ndani ya daladala katikati ya wiki hii jijini humo.


PHOTO: Haina uhusiano na tukio katika habari hii.

Mwandishi wa habari hii ambaye alikuwemo ndani ya gari hilo ambayo redio ya ndani ya gari hiyo ilikuwa ikitangaza (Clouds fm) habari za nyoka huyo ambaye alioneka kwenye gari lenye namba za usajili T184 DDJ lililokuwa likifanya safari zake kutoka Kibamba na Makumbusho jijiji Dar, hivyo kupelekea abilia waliokuwa wamekaa kugoma kuwabebea mikoba abilia waliokuwa wamesimama.

Msomaji wa taarifa hiyo alipomaliza kusoma baadhi ya abilia walianza kukaguana kuona iwapo ndani ya daladala hilo kuna aliyebeba begi kubwa linaloweza kuhifadhi mdudu huyo, ambapo watu wengi waliokuwemo kwenye daladala hilo walionyesha kushtushwa  na taarifa hiyo.

Wakati watu kadhaa walihusisha tukio hilo na Imani za kishirikina wengine walisema huenda mmiliki wa joka hilo alikuwa akilifuga. Katika tukio la daladala la Kibamba abiria waliokuwa ndani ya gari hilo walisema tukio hilo la kutisha lilisababisha abilia kutaka kuruka wakati likiwa kwenye mwendo wa kasi.




Source: Tanzania Daima.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top