0
Tukio la kutekwa nyara kwa msanii wa nyimbo za bongo freva Ibrahim Musa maarufu kama Roma Mkatoliki na wenzake wanne waliokuwa Studio za Tongwe Records iliyopo masaki Dar Es Salaam wakifanya kazi ya kurekodi nyimbo umefanyika ndani ya muda mfupi wa dakika 15 ambao watekaji aliutumia kuingia na kuwachukua wasanii hao.

PROFILE PHOTO: Ibrahim Musa aka Roma Mkatoliki.

Watu hao ambao walikuwa na siraha waliondoka na mateka huku wakitumia gari aina ya Toyota Noah ambayo shuhuda wa tukio hilo aliyejulikana kwa jina maarufu Ze City alisema jinsi utekaji huo ulivyofanyika.
Haika Shabani au ‘Ze City’ alisema watekaji hao walifika katika studio hizo majira ya saa 12:30 jioni na kuongea na Roma kwa takribani robo saa na waliondoka saa 12:45 baada ya kumuingiza Roma na wenzake kwenye gari iliyokuwa na rangi nyeupe.

“Nilipokuwa nashuka kwenye bajaji, ikaja gari nyuma yangu, ikashusha watu watano, wakatuamuru tuliokuwa nje nikiwamo mimi, producer na watu wengine wawili tuingie ndani, baadaye walituambia bila kujitambulisha kuwa wamekuja kumtafuta J Murder ambaye ni mmiliki wa studio hiyo na Roma, wakaambiwa wamemkosa mmiliki ila Roma yupo” alisema Ze City.

Aliongeza kuwa “baada ya kuitiwa Roma na kutoka naye nje na kuingia naye kwenye gari, wachache waliingia studio na walipotoka walibeba TV na CD zilizokuwepo pale ambapo baadaye walirudi naye ndani na kuchukua baadhi ya vitu kama camera na kuondoka na watu wawili akiwamo mlinzi na msanii aliyefahamika kwa jina la Moni.”

Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar Es Salaam Simon siro tayari aliunda kamati maalum kufuatilia na kucunguza tukio hilo, huku zikiwa tayari zimetimia siku mbili tangu msanii huyo kutekwa. Wakati huohuo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imetoa taarifa kwa vyombo vya habari kuwa inafuatilia kwa karibu suala hilo na imebaini ni la kijinai.

Vilevile hapo jana wasanii wapatao 30 waliungana kupaza sauti zao kutaka mamlaka husika zichukue hatua stahiki ikiwa ni zaidi ya saa 40 kupita tangu alipotekwa muimbaji huyo wa nyimbo za kufoka.                
                                                                                                           Source: Mwananchi

PROFILE PHOTO: Kamanda wa Polisi kanda
maalum ya Dar Es Samaa Simon Siro.
Mara baada ya tukio hilo kugusa hisia za watu mbalimbali Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar Es Salaam Simon Siro ametoa taarifa na kuwa  leo asubuhi katika kituo cha polisi Oystebay  jijini Dar Es Salaam mwanamuziki huyo Roma Mkatoliki alifika katika kituo hicho mara baada ya kuachiwa na watekaji hao.

“Baada ya yale mahojiano wengine wakawa wanawahoji kwa kutumia nguvu, wana majeraha kidogo ambayo yameonekana hivyo baada ya kuwahoji wameonekana kupaniki wamechukuliwa maelezo yao na nimeelekeza wapilekwe hospitali na askali wetu wa upelelezi.” Amesema Kamanda Siro.

Aliongeza kuwa “kimsingi niseme kuwa wote wanne wamepatikana wakiwa salama na upelelezi wa kina unaendelea kwa wote waliohusika na hilo tukio ingawa wanasema hawakuwatambua lakini zile zilikuwa taarifa za awali baada ya kuwa watakuwa wametulia watatupeleka katika eneo la tukio tuendelee na upelelezi na baadaye tutajua kwa undani kuhusu tukio hili.”

LATEST: Muda mfupi baada ya kutoka hospitali, mwanamuziki huyo alisema "Mimi ni mzima kabisa kiafya" ikiwa ni baada ya kufanyiwa vipimo katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar Es Salaam ambapo amesema atazungumza mengi siku ya Jumatatu.


Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top